Ameacha Twawaaf ya kuaga kwa sababu ya ujinga

Swali: Nilitekeleza faradhi ya Hajj mwaka uliopita na nilipomaliza matendo ya Hajj nilienda Tan‘iym, nikahirimia ´Umrah, nikaingia ndani ya Haram, nikatekeleza matendo ya ´Umrah ya Twawaaf, Sa‘y na kunyoa. Kisha nikaondoka wakati huohuo kutoka Makkah al-Mukarramah bila kufanya Twawaaf ya kuaga kwa ujinga wangu, kwa sababu nilidhani kuwa Twawaaf ya ´Umrah inanitosha. Ni ipi hukumu?

Jibu: Inatosha. Maadamu ulifanya Twawaaf, ukafanya Sa‘y na ukaondoka mara moja, inatosha. Twawaaf ya ´Umrah inatosha, kama ilivyokuja katika Hadiyth ya ‘Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) kwamba alifanya Twawaaf kwa ajili ya ´Umrah yake kisha akaondoka pamoja na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wala haikutajwa kwamba alifanya Twawaaf baada ya Twawaaf ya ´Umrah.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1934/حكم-من-حج-ثم-اعتمر-ثم-سافر-ولم-يطف-طواف-الوداع
  • Imechapishwa: 04/07/2026