Allaah atampa thabati kila ambaye ni muumini

Swali: Imethibiti katika Hadiyth Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kuwa kila muumini atasoma kwenye paji la uso la ad-Dajjaal ´kafiri`. Je, katika haya kuna dalili inayoonesha kuwa mtu ambaye si msomi Atathibitishwa na Allaah ikiwa ni muumini?

Jibu: Ndio. Ambaye si msomi Atathibitishwa:

يُثَبِّتُ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا

“Allaah Huwathibitisha wale walioamini kwa kauli thabiti.” (14:27)

Hili ni kwa watu wote, sawa mtu akiwa ni msomi au si msomi. Linamuhusu kila muumini.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Kitaab Ahaadiyth-il-Fitnah http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/hadist%20fitan-17-08-1435-01.mp3
  • Imechapishwa: 21/04/2015