“Allaah akuhifadhi kwa jaha ya Mtume”

Swali: Ni ipi hukumu ya kusema:

“Allaah akuhifadhi kwa jaha ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)”?

Jibu: Sema:

“Allaah akuhifadhi.”

Inatosha. Allaah hana haja ya jaha ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Yeye (Subhaanahu wa Ta´ala) anakuhifadhi pasi na jaha ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hii ni Bid´ah. Kwa sababu kuomba kwa jaha ni jambo halikuthibiti katika Qur-aan, Sunnah wala katika maneno ya Salaf. Ni njia miongoni mwa njia za shirki. Utaanza kuomba msaada kwa jaha kidogo kidogo mpaka umuombe msaada na kumuomba yeye. Hii ni njia miongoni mwa njia za shirki. Kitendo hichi ni Bid´ah na ni njia miongoni mwa njia za shirki. Kuomba kwa jaha, haki au kwa mtu mwenyewe. Yote haya hayajuzu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Nawaaqidh-il-Islaam (09) http://ajurry.com/safrawy/chorohat-elakida/chorohat-nawakid-elislam/charh-salah-fawzan/09.mp3
  • Imechapishwa: 31/03/2019