Swali: Mtu akimtaliki mke wake mara tatu katika kikao kimoja inahesabika ni talaka tatu au moja?
Jibu: Inahesabiwa ni talaka moja. Muslim amepokea katika “as-Swahiyh” kupitia kwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ambaye amesema:
“Talaka tatu zilikuwa zinahesabiwa ni talaka moja wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), wakati wa Abu Bakr na wakati wa ´Umar.”
Kuna kipindi ´Umar alikuwa anaona kuwa zote tatu zinapita. Hata hivyo Sunnah ya Mtume wa Allaah wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ina haki zaidi ya kufuatwa. ash-Shawkaaniy amesema:
“Maimamu wanne wamechukua maoni ya ´Umar. Ikiwa mmeacha Sunnah kwa ajili yake ´Umar, anaangukia wapi masikini huyu mbele ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)? Ikiwa mnaiacha Sunnah kwa ajili ya madhehebu, ni yenye kudharauliwa zaidi kuliko kuyapinganisha na Sunnah za Mtume wa Allaah wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?”[1]
[1] Nayl-ul-Awtwaar.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 296
- Imechapishwa: 09/08/2025
Swali: Mtu akimtaliki mke wake mara tatu katika kikao kimoja inahesabika ni talaka tatu au moja?
Jibu: Inahesabiwa ni talaka moja. Muslim amepokea katika “as-Swahiyh” kupitia kwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ambaye amesema:
“Talaka tatu zilikuwa zinahesabiwa ni talaka moja wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), wakati wa Abu Bakr na wakati wa ´Umar.”
Kuna kipindi ´Umar alikuwa anaona kuwa zote tatu zinapita. Hata hivyo Sunnah ya Mtume wa Allaah wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ina haki zaidi ya kufuatwa. ash-Shawkaaniy amesema:
“Maimamu wanne wamechukua maoni ya ´Umar. Ikiwa mmeacha Sunnah kwa ajili yake ´Umar, anaangukia wapi masikini huyu mbele ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)? Ikiwa mnaiacha Sunnah kwa ajili ya madhehebu, ni yenye kudharauliwa zaidi kuliko kuyapinganisha na Sunnah za Mtume wa Allaah wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?”[1]
[1] Nayl-ul-Awtwaar.
Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 296
Imechapishwa: 09/08/2025
https://firqatunnajia.com/al-waadiiy-kuhusu-talaka-tatu-kwa-mpigo/