Swali: Ni ipi hali ya Shaykh Ibraahiym ar-Ruhayliy?

Jibu: Ibraahiym ar-Ruhayliy ana makosa mengi – Allaah atusamehe sisi na yeye. Ana makosa 13 au zaidi. Yule atakayesoma Radd yangu kwake atayaona. Hata hivyo sikutaja makosa yote. Miongoni mwa makosa hayo ni kumtetea kwake al-Qaasimiy na kwamba ni katika Ahl-us-Sunnah na Mujtahid.

Kosa lingine ni maneno yake aliposema kuwa yeye hakatazi kuchukua elimu kwa mtu ambaye hamfanyii Tabdiy´ al-Jahm bin Swafwaan – mtu ambaye kuna maafikiano juu ya ukafiri wake. Ana majanga mengi.

Laiti mimi ningelisema hivo, au baadhi ya maneno yake, basi ingelazimika kunitahadharisha.

  • Mhusika: Shaykh ´Ubayd bin ´Abdillaah al-Jaabiriy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=137224
  • Imechapishwa: 13/11/2022