Saudi Arabia imejengwa juu ya ´Aqiydah sahihi na mfumo wa Salaf. Hawakubali kitu chochote kisichostahiki na utata kutoka kwa wajinga au mwanachuoni lakini mpotevu ambaye anakusudia kubadilisha mwelekeo wa nchi na kuingiza fikira zinazoenda kinyume na ´Aqiydah sahihi na mfumo uliosalama ambao inafuata.

Yeyote anayejaribu kufanya hivo wanachuoni wa nchi wamemraddi na kumuondoa. Miongoni mwa hao ni yale ambayo ndugu na Shaykh ´Abdullaah bin Muhammad bin ´Aamir al-Ahmariy ameandika kwa jina “an-Nuquulaat as-Salafiyyah fiyr-Radd ´alaal-Haddaadiyyah”. Kitabu kimezungumzia Takfiyr, Tadhwliyl na Tabdiy´. Radd yake imefunua utata wao na kufuta makosa yao kikamilifu.

Allaah Amjaze kheri na Amnufaishe kwa yale aliyoandika na kubainisha.

  • Mhusika: Imeandikwa na: Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Utangulizi wa “an-Nuquulaat as-Salafiyyah fiyr-Radd ´alaa at-Twaaifah al-Haddaadiyyah”, uk. 9-10