Swali: Tunasikia kuhusu Da´wah Yemen inayofanywa na Shaykh Muqbil al-Waadi´iy na kwamba ni nusura ya Da´wah ya Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) kwa sababu alichota elimu kutoka katika nchi hii. Unasemaje juu ya hili?

Jibu: Ndio. Shaykh Muqbil (Rahimahu Allaah) alisoma katika nchi hii na kwenye chuo kikuu cha Kiislamu. Alijifunza Tawhiyd na akarudi Yemen. Alilingania kwa Allaah na katika Tawhiyd. Da´wah yake ni nzuri kutokana na tulivyosikia na kutokana na yale matunda iliyozalisha. Allaah amenufaisha kupitia kwake. Allaah amrehemu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://hatrashy.twheed.net/download.php?id=91
  • Imechapishwa: 11/11/2022