Swali: Wako ambao wanasema kwamba maoni ya Shaykh al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) katika imani ni yaleyale kama ya Murji-ah. Unasemaje juu ya hilo?
Jibu: al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) ni mwanachuoni, Muhaddith na Faqiyh, hata kama alikuwa mwenye nguvu zaidi katika Hadiyth kuliko Fiqh.
Sijui kuwa ana maoni yenye kufahamisha juu ya Irjaa´. Lakini wanaotaka kuwakufurisha watu husema juu yake na kwa watu mfano wake kwamba ni Murji-ah. Inahusiana na kupeana majina bandia. Mimi nashuhudia juu ya Shaykh al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) juu ya kuwa na msimamo, ´Aqiydah salama na makusudio mazuri.
Lakini pamoja na hivyo sisemi kuwa hakosei. Kwa sababu hakuna yeyote, baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye amekingwa na kukosea.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-As-ilah al-Qatwariyyah, uk. 18-19
- Imechapishwa: 16/02/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)