as-Safaariyniy amesema:
“Ahl-us-Sunnah ni makundi matatu: Athariyyah linaloongozwa na Ahmad bin Hanbal, Ashaa´irah linaloongozwa na Abul-Hasan al-Ash´ariy na Maaturiydiyyah linaloongozwa na Abu Mansuur al-Maaturiydiy. Ama kuhusiana na makundi potofu, ni mengi sana.”[1]
Kuwagawa Ahl-us-Sunnah katika makundi matatu ni jambo linatakiwa kujadiliwa. Ahl-us-Sunnah pasi na shaka yoyote ni kundi moja ambalo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amelieleza kwa kusema:
“Ni mkusanyiko.”
Katika upokezi mwingine amesema:
“Ni lile litakalofuata yale ninayofuata mimi hii leo na Maswahabah zangu.”
au:
“Ni lile litakalofuata yale ninayofuata mimi na Maswahabah zangu.”
Mtu anapata kufahamu kwamba ni wenye kuafikiana juu yale aliyokuwemo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na Maswahabah zake. Kwa hivyo ni kundi moja. Mwandishi mwenyewe (Rahimahu Allaah) amesema katika utangulizi wa shairi lake wakati alipotaja Hadiyth hii:
“Maandiko haya hayalihusu kundi lingine isipokuwa Ahl-ul-Athar.”[2]
Bi maana Athariyyah. Hivyo basi mtu anapata kufahamu kuwa Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni kundi moja, nalo ni Athariyyah – na Allaah ndiye mjuzi zaidi.
[1] Lawaamiy´-ul-Anwaar al-Bahiyyah (1/73).
[2] Abu Daawuud (4596) na at-Tirmidhiy (2641) kutoka kwa Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa). Nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”al-Mishkaah” (171).
- Mhusika: Imaam ´Abdullaah bin ´Abdir-Rahmaan Abaa Butwayn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Haashiyah ´alaa Lawaamiy´-il-Anwaar al-Bahiyyah (1/73)
- Imechapishwa: 06/03/2019
as-Safaariyniy amesema:
“Ahl-us-Sunnah ni makundi matatu: Athariyyah linaloongozwa na Ahmad bin Hanbal, Ashaa´irah linaloongozwa na Abul-Hasan al-Ash´ariy na Maaturiydiyyah linaloongozwa na Abu Mansuur al-Maaturiydiy. Ama kuhusiana na makundi potofu, ni mengi sana.”[1]
Kuwagawa Ahl-us-Sunnah katika makundi matatu ni jambo linatakiwa kujadiliwa. Ahl-us-Sunnah pasi na shaka yoyote ni kundi moja ambalo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amelieleza kwa kusema:
“Ni mkusanyiko.”
Katika upokezi mwingine amesema:
“Ni lile litakalofuata yale ninayofuata mimi hii leo na Maswahabah zangu.”
au:
“Ni lile litakalofuata yale ninayofuata mimi na Maswahabah zangu.”
Mtu anapata kufahamu kwamba ni wenye kuafikiana juu yale aliyokuwemo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na Maswahabah zake. Kwa hivyo ni kundi moja. Mwandishi mwenyewe (Rahimahu Allaah) amesema katika utangulizi wa shairi lake wakati alipotaja Hadiyth hii:
“Maandiko haya hayalihusu kundi lingine isipokuwa Ahl-ul-Athar.”[2]
Bi maana Athariyyah. Hivyo basi mtu anapata kufahamu kuwa Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni kundi moja, nalo ni Athariyyah – na Allaah ndiye mjuzi zaidi.
[1] Lawaamiy´-ul-Anwaar al-Bahiyyah (1/73).
[2] Abu Daawuud (4596) na at-Tirmidhiy (2641) kutoka kwa Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa). Nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”al-Mishkaah” (171).
Mhusika: Imaam ´Abdullaah bin ´Abdir-Rahmaan Abaa Butwayn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Haashiyah ´alaa Lawaamiy´-il-Anwaar al-Bahiyyah (1/73)
Imechapishwa: 06/03/2019
https://firqatunnajia.com/ahl-us-sunnah-ni-kundi-moja/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)