Swali: Nini hukumu ya adhaana inayotolewa na mwenye kutenda dhambi nzito?
Jibu: Maoni yaliyotagaa kati ya wanazuoni ni kwamba haisihi. Ni lazima muadhini awe mtu mwadilifu, ijapo kwa muonekano wa nje. Kwa sababu anatoa taarifa ya wakati wa swalah. Taarifa za watenda madhambi mazito hazikubaliwi. Ni lazima awe mwadilifu. Hata hivyo ikiwa kuna waadhini wengine katika mji wanaosikika na wanatosheleza, basi jambo hili ni jepesi zaidi. Hali ya kuwepo kwake ni sawa na kutokuwepo kwake. Lakini haifai kumpa jukumu la kutoa adhaana mahali ambapo watu wanamtegemea. Kwa hali yoyote haifai kabisa kumpa jukumu hili mtu ambaye ufisadi wake umebainika wazi. Haijuzu kupewa jukumu hilo.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24787/حكم-اذان-الفاسق
- Imechapishwa: 23/12/2024
Swali: Nini hukumu ya adhaana inayotolewa na mwenye kutenda dhambi nzito?
Jibu: Maoni yaliyotagaa kati ya wanazuoni ni kwamba haisihi. Ni lazima muadhini awe mtu mwadilifu, ijapo kwa muonekano wa nje. Kwa sababu anatoa taarifa ya wakati wa swalah. Taarifa za watenda madhambi mazito hazikubaliwi. Ni lazima awe mwadilifu. Hata hivyo ikiwa kuna waadhini wengine katika mji wanaosikika na wanatosheleza, basi jambo hili ni jepesi zaidi. Hali ya kuwepo kwake ni sawa na kutokuwepo kwake. Lakini haifai kumpa jukumu la kutoa adhaana mahali ambapo watu wanamtegemea. Kwa hali yoyote haifai kabisa kumpa jukumu hili mtu ambaye ufisadi wake umebainika wazi. Haijuzu kupewa jukumu hilo.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24787/حكم-اذان-الفاسق
Imechapishwa: 23/12/2024
https://firqatunnajia.com/adhaana-ya-fasiki/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)