´Abdul-Hamiyd Kishk – mpiga visa

Kwa hakika ni kwamba, kisa hichi ulichohadithia kutoka kwa mtu huyu [Kishk], sijawahi kukipitia, si katika Hadiyth Swahiyh, Hasan, dhaifu, ya kuundwa wala zisizokuwa na asili.

Ukweli mwingine na ambao unasikitisha, ni kwamba huyu Shaykh Kishk, haikataliwi kamwe ya kwamba usulubu wake wa kuathiri watu wa kawaida ni usulubu wa ajabu. Lakini simaanishi ya kwamba usulubu huu ni usulubu wa Kishari´ah. Kwa kuwa anatumia hisia za hali ya juu na kuamsha hisia za wenye kumsikiliza. Kwa mfano katika kumsalia Mtume, anasema:

“Hebu nisikilizeni na kadhalika!”

Lakini mwisho wake usulubu wake ni wenye kuathiri. Lakini kwa masikitiko makubwa, naitakidi ya kuwa ni mpiga visa na sio mwanachuoni. Na khaswa kuhusian na elimu ya Hadiyth za Mtume. Na haitoshi ya kuwa ni mpiga visa tu. Huleta pia Hadiyth za kila aina na kila kona na kuwatolea mawaidha watu na kuwakumbusha kwa kutumia Hadiyth hizo.

  • Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Silsilat-ul-Hudaa wan-Nuur (195)
  • Imechapishwa: 28/07/2020