Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
Amesema tena:
“Nywele zake timtim na miguu yake imeingia vumbi. Ananyoosha mikono yake kuelekea mbinguni akisema: “Ee Mola! Ee Mola!”[1]
MAELEZO
Hadiyth hii inahusu yule msafiri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Enyi watu! Hakika Allaah ni mzuri na wala hakubali isipokuwa kilicho kizuri. Allaah amewaamrisha waumini yale aliyowaamrisha Mitume. Akasema:
يَا أَيُّهَا الرُّسُلُ كُلُوا مِنَ الطَّيِّبَاتِ وَاعْمَلُوا صَالِحًا ۖ إِنِّي بِمَا تَعْمَلُونَ عَلِيمٌ
“Enyi Mitume! Kuleni katika vizuri na tendeni mema – hakika Mimi kwa yale myatendayo ni Mjuzi.”[2]
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُلُوا مِن طَيِّبَاتِ مَا رَزَقْنَاكُمْ
“Enyi walioamini! Kuleni vizuri Tulivyokuruzukuni.”[3]
Baada ya hapo akamtaja bwana mmoja ambaye amesafiri safari ndefu. Nywele zake zimekuwa timtim na miguu yake imeingia vumbi. Ananyoosha mikono yake kuelekea mbinguni akisema: “Ee Mola! Ee Mola!” Chakula chake ni cha haramu, mavazi yake ni ya haramu na amekulia juu ya haramu; ni vipi ataitikiwa?”
Anamnyooshea mikono Allaah (Jalla wa ´Alaa), kwa sababu Allaah yuko juu ya mbingu. Anamnyooshea mikono Allaah, Aliye juu, akisema:
“Ee Mola! Ee Mola!”
Anakariri du´aa yake na akifanya king´ang´anizi, jambo ambalo ni miongoni mwa sababu za kuitikiwa du´aa. Hata hivyo licha ya kuwa yuko na sababu hizi za kuitikiwa du´aa – yuko safarini, mazingira yake ni mabaya kutokana na safari, ananyoosha mikono yake kuelekea mbinguni na anaikariri du´aa yake na kung´ang´ania – du´aa yake haijibiwi. Kikwazo ni “chakula chake ni cha haramu, mavazi yake ni ya haramu na amekulia juu ya haramu”. Hakula chakula kizuri na chenye kunufaisha. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَيُحِلُّ لَهُمُ الطَّيِّبَاتِ وَيُحَرِّمُ عَلَيْهِمُ الْخَبَائِثَ
“… anawahalalishia vilivyo vizuri na anawaharamishia vichafu… ”[4]
Huyu hakula katika vilivyo vizuri. Ndio maana du´aa yake haikuitikwa. Jumla isemayo ”Ananyoosha mikono yake kuelekea mbinguni akisema: “Ee Mola! Ee Mola!” inathibitisha kuwa Allaah yuko juu ya viumbe Wake.
[1] Muslim (1015).
[2] 23:51
[3] 2:172
[4] 7:157
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat at-Tawdhwiyhiyyah ´alaa Muqaddimat-il-Fatwaa al-Hamawiyyah, uk. 134-135
- Imechapishwa: 28/08/2024
Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
Amesema tena:
“Nywele zake timtim na miguu yake imeingia vumbi. Ananyoosha mikono yake kuelekea mbinguni akisema: “Ee Mola! Ee Mola!”[1]
MAELEZO
Hadiyth hii inahusu yule msafiri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Enyi watu! Hakika Allaah ni mzuri na wala hakubali isipokuwa kilicho kizuri. Allaah amewaamrisha waumini yale aliyowaamrisha Mitume. Akasema:
يَا أَيُّهَا الرُّسُلُ كُلُوا مِنَ الطَّيِّبَاتِ وَاعْمَلُوا صَالِحًا ۖ إِنِّي بِمَا تَعْمَلُونَ عَلِيمٌ
“Enyi Mitume! Kuleni katika vizuri na tendeni mema – hakika Mimi kwa yale myatendayo ni Mjuzi.”[2]
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُلُوا مِن طَيِّبَاتِ مَا رَزَقْنَاكُمْ
“Enyi walioamini! Kuleni vizuri Tulivyokuruzukuni.”[3]
Baada ya hapo akamtaja bwana mmoja ambaye amesafiri safari ndefu. Nywele zake zimekuwa timtim na miguu yake imeingia vumbi. Ananyoosha mikono yake kuelekea mbinguni akisema: “Ee Mola! Ee Mola!” Chakula chake ni cha haramu, mavazi yake ni ya haramu na amekulia juu ya haramu; ni vipi ataitikiwa?”
Anamnyooshea mikono Allaah (Jalla wa ´Alaa), kwa sababu Allaah yuko juu ya mbingu. Anamnyooshea mikono Allaah, Aliye juu, akisema:
“Ee Mola! Ee Mola!”
Anakariri du´aa yake na akifanya king´ang´anizi, jambo ambalo ni miongoni mwa sababu za kuitikiwa du´aa. Hata hivyo licha ya kuwa yuko na sababu hizi za kuitikiwa du´aa – yuko safarini, mazingira yake ni mabaya kutokana na safari, ananyoosha mikono yake kuelekea mbinguni na anaikariri du´aa yake na kung´ang´ania – du´aa yake haijibiwi. Kikwazo ni “chakula chake ni cha haramu, mavazi yake ni ya haramu na amekulia juu ya haramu”. Hakula chakula kizuri na chenye kunufaisha. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَيُحِلُّ لَهُمُ الطَّيِّبَاتِ وَيُحَرِّمُ عَلَيْهِمُ الْخَبَائِثَ
“… anawahalalishia vilivyo vizuri na anawaharamishia vichafu… ”[4]
Huyu hakula katika vilivyo vizuri. Ndio maana du´aa yake haikuitikwa. Jumla isemayo ”Ananyoosha mikono yake kuelekea mbinguni akisema: “Ee Mola! Ee Mola!” inathibitisha kuwa Allaah yuko juu ya viumbe Wake.
[1] Muslim (1015).
[2] 23:51
[3] 2:172
[4] 7:157
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Ta´liyqaat at-Tawdhwiyhiyyah ´alaa Muqaddimat-il-Fatwaa al-Hamawiyyah, uk. 134-135
Imechapishwa: 28/08/2024
https://firqatunnajia.com/92-ndio-maana-hakuitikiwa-duaa-yake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)