Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
´Abdullaah bin Rawaahah (Radhiya Allaahu ´anh) alisema kumwambia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
Nashuhudia kwamba ahadi ya Allaah ni haki
na kwamba Moto ni makazi ya makafiri
na kwamba ´Arshi iko juu ya maji
na kwamba juu ya ´Arshi yuko Mola wa walimwengu
inabebwa na Malaika watukufu
na Malaika wa Mungu ni wenye kuleta upepo
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamkubalia maneno yake[1].
MAELEZO
Miongoni mwa maneno ya Maswahabah yanayothibitisha kuwepo juu kwa Allaah ni maneno ya ´Abdullaah bin Rawaahah al-Answaariy (Radhiya Allaahu ´anh). Alikuwa mshairi fasaha na mmoja katika washairi wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Aliutetea Uislamu na akawaraddi washirikina kwa mashairi yake. Kama mfano wa Hassaan bin Thaabit, Ka´b bin Maalik na Ka´b bin Zuhayr (Radhiya Allaahu ´anhum); hawa ni washairi waliyoyatumia mashairi yao kumtetea Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wakawaraddi washirikina.
Kisa chake ni kwamba alikuwa na kijakazi aliyekuwa akilala naye. Siku moja akaja mke wake na akashikwa na wivu kama wanawake wengine. Kwa ajili ya kuepuka matatizo, akakanusha kuwa amefanya kitu na kijakazi yule ambapo mke wake akamwambia ambaye yuko na janaba haifai kwake kusoma Qur-aan; soma Qur-aan kama kweli hujafanya kitu! Ndipo akamfanyia Tawriyah kwa njia ya kwamba akayasoma mashairi hapo juu ambapo mwanamke yule akafikiria kuwa ni Qur-aan. Mwanamke yule akamsadikisha. Hii ni Tawriyah. Inafaa kwa mtu kufanya Tawriyah akiwa si mwenye kudhulumu. Akamsadikisha na kusema kuwa anamwamini Allaah na kuyakadhibisha macho yake. Baada ya hapo tukio hilo akaelezwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambapo akamkubalia kitendo chake.
Kinacholengwa katika mashairi hayo ni “kwamba juu ya ´Arshi yuko Mola wa walimwengu” ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamkubalia. Akamkubalia jumla inayosema kuwa ´Arshi iko juu ya maji na kwamba Allaah yuko juu ya ´Arshi.
[1] al-Istiy´aab kwenye ”al-Iswaabah” (2/296) ya Ibn Hajar.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat at-Tawdhwiyhiyyah ´alaa Muqaddimat-il-Fatwaa al-Hamawiyyah, uk. 129-130
- Imechapishwa: 27/08/2024
Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
´Abdullaah bin Rawaahah (Radhiya Allaahu ´anh) alisema kumwambia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
Nashuhudia kwamba ahadi ya Allaah ni haki
na kwamba Moto ni makazi ya makafiri
na kwamba ´Arshi iko juu ya maji
na kwamba juu ya ´Arshi yuko Mola wa walimwengu
inabebwa na Malaika watukufu
na Malaika wa Mungu ni wenye kuleta upepo
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamkubalia maneno yake[1].
MAELEZO
Miongoni mwa maneno ya Maswahabah yanayothibitisha kuwepo juu kwa Allaah ni maneno ya ´Abdullaah bin Rawaahah al-Answaariy (Radhiya Allaahu ´anh). Alikuwa mshairi fasaha na mmoja katika washairi wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Aliutetea Uislamu na akawaraddi washirikina kwa mashairi yake. Kama mfano wa Hassaan bin Thaabit, Ka´b bin Maalik na Ka´b bin Zuhayr (Radhiya Allaahu ´anhum); hawa ni washairi waliyoyatumia mashairi yao kumtetea Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wakawaraddi washirikina.
Kisa chake ni kwamba alikuwa na kijakazi aliyekuwa akilala naye. Siku moja akaja mke wake na akashikwa na wivu kama wanawake wengine. Kwa ajili ya kuepuka matatizo, akakanusha kuwa amefanya kitu na kijakazi yule ambapo mke wake akamwambia ambaye yuko na janaba haifai kwake kusoma Qur-aan; soma Qur-aan kama kweli hujafanya kitu! Ndipo akamfanyia Tawriyah kwa njia ya kwamba akayasoma mashairi hapo juu ambapo mwanamke yule akafikiria kuwa ni Qur-aan. Mwanamke yule akamsadikisha. Hii ni Tawriyah. Inafaa kwa mtu kufanya Tawriyah akiwa si mwenye kudhulumu. Akamsadikisha na kusema kuwa anamwamini Allaah na kuyakadhibisha macho yake. Baada ya hapo tukio hilo akaelezwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambapo akamkubalia kitendo chake.
Kinacholengwa katika mashairi hayo ni “kwamba juu ya ´Arshi yuko Mola wa walimwengu” ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamkubalia. Akamkubalia jumla inayosema kuwa ´Arshi iko juu ya maji na kwamba Allaah yuko juu ya ´Arshi.
[1] al-Istiy´aab kwenye ”al-Iswaabah” (2/296) ya Ibn Hajar.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Ta´liyqaat at-Tawdhwiyhiyyah ´alaa Muqaddimat-il-Fatwaa al-Hamawiyyah, uk. 129-130
Imechapishwa: 27/08/2024
https://firqatunnajia.com/89-wakati-ibn-rawaahah-aliposhtukiziwa-na-kijakazi-wake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)