Pepo na Moto havitomalizika. Amesema (Ta´ala):
جَزَاؤُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتُ عَدْنٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا
“Malipo yao yako kwa Mola wao; mabustani ya kudumu milele yapitayo chini yake mito hali ya kuwa ni wenye kudumu humo milele.”[1]
Aayah zinazosema kuwa Moto utakuwa milele ni nyingi. Kuhusu Moto yametajwa hayo maeneo matatu. Katika “an-Nisaa´”:
وَلَا لِيَهْدِيَهُمْ طَرِيقًا إِلَّا طَرِيقَ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا
“… wala kuwaongoza njia; isipokuwa njia ya Jahannam wadumishwe humo milele.”[2]
Katika “al-Ahzaab”:
إِنَّ اللَّـهَ لَعَنَ الْكَافِرِينَ وَأَعَدَّ لَهُمْ سَعِيرًا خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا
“Hakika Allaah Amewalaani makafiri, na Amewaandalia moto uliowashwa vikali mno. Ni wenye kudumu humo abadi.”[3]
Katika “al-Jinn:
وَمَن يَعْصِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ فَإِنَّ لَهُ نَارَ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا
“Yeyote atakayemuasi Allaah na Mtume Wake, basi hakika atapata Moto wa Jahannam hali ya kudumu humo milele.”[4]
Allaah (Ta´ala) amesema:
إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي عَذَابِ جَهَنَّمَ خَالِدُونَ لَا يُفَتَّرُ عَنْهُمْ وَهُمْ فِيهِ مُبْلِسُونَ
”Hakika wahalifu wamo kwenye adhabu ya [Moto wa] Jahannam watadumu milele. Hawatopumzishwa nayo nao humo watakata tamaa.”[5]
[1] 98:08
[2] 04:168-169
[3] 33:64-65
[4] 72:23
[5] 43:74-75
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 132
- Imechapishwa: 12/12/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)