Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Hadiyth Swahiyh:
“Wakati Allaah (´Azza wa Jall) alipohukumu viumbe aliandika katika kitabu Chake kilichoko Kwake juu ya ´Arshi: ”Hakika huruma Yangu inashinda ghadhabu Zangu.”[1]
MAELEZO
Hadiyth inafahamisha kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) yuko juu ya ´Arshi. ´Arshi ndio kiumbe kilicho juu kabisa; hakuna kiumbe chochote kilichoko juu ya ´Arshi. Allaah (´Azza wa Jall) yuko juu ya ´Arshi ujuu ambao unalingana na utukufu Wake. Haina maana kuwa anahitaji ´Arshi hiyo au kwamba ´Arshi inambeba – bali Yeye (Subhaanahu wa Ta´ala) ndiye ambaye anaizuia ´Arshi kwa uwezo Wake.
Hadiyth inathibitisha pia kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) anaandika.
Inafahamisha pia kwamba wako baadhi ya viumbe walioko Kwake kwa njia ya nafasi na matukuzo. Kama alivosema Allaah (Ta´ala):
إِنَّ الَّذِينَ عِندَ رَبِّكَ لَا يَسْتَكْبِرُونَ عَنْ عِبَادَتِهِ وَيُسَبِّحُونَهُ وَلَهُ يَسْجُدُونَ
“Hakika wale walioko kwa Mola wako hawatakabari kufanya ‘ibaadah Yake na wanamsabihi na Kwake pekee wanasujudu.”[2]
[1] al-Bukhaariy (3194), Muslim (2751), Ahmad (2/466) na wengineo.
[2] 7:206
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat at-Tawdhwiyhiyyah ´alaa Muqaddimat-il-Fatwaa al-Hamawiyyah, uk. 127
- Imechapishwa: 26/08/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket