Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Ndio maana hawa wajinga wanatakiwa kuambiwa: “Ni jambo linalojulikana ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwapiga vita mayahudi na akawafanya mateka licha ya kuwa wao wanasema “Hakuna mungu wa haki isipokuwa Allaah”. Kadhalika Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walipigana vita na Banuu Haniyfah pamoja na kuwa wanasema ” Hakuna mungu wa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah”, wanaswali na kudai Uislamu. Vilevile wale aliowaunguza kwa moto ´Aliy bin Abiy Twaalib.
MAELEZO
Haya ni majibu juu ya shubuha zilizotangulia walizoleta wajinga hawa. Majibu yako ifuatavyo:
1 – Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwapiga vita mayahudi na akawafanya mateka licha ya kuwa wanasema hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah.
2 – Maswahabah waliwapiga vita Banuu Haniyfah pamoja na kwamba wanashuhudia ya kwamba hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah, wanaswali na kudai kuwa ni waislamu.
3 – Wale ambao ´Aliy bin Abiy Twaalib aliwachoma kwa moto walikuwa wakishuhudia pia kwamba hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 92
- Imechapishwa: 28/11/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket