81 – ´Aarim bin al-Fadhwl ametuhadithia: ´Abdullaah bin al-Mubaarak ametuhadithia: Zakariyyaa ametuhadithia, kutoka kwa Wahb bin al-Ajda´: Nimemsikia ´Umar bin al-Khattwaab akisema:
”Mnapofika, basi tufuni kwenye Ka´bah mara saba na swalini Mahali pa kusimama Rak´ah mbili. Kisha nendeni Swafaa na simameni pale mnapoweza kuiona Nyumba. Pigeni Takbiyr saba. Baina ya kila Takbiyr kuna himdi na sifa kwa Allaah, kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kujiomba du´aa mwenyewe. Fanya mfano wa hivo Marwah.”[1]
[1] Cheni ya wapokezi ni Swahiyh. ´Aarim, ambaye jina lake ni Muhammad bin al-Fadhwl (´Aarim ilikuwa ni jina lake la utani), ameihifadhi. Kumbukumbu yake ilibadilika muda ulivyoenda. Wapokezi wake wengine waliobaki ni waaminifu. Ibn-ul-Qayyim ameitaja katika “Jalaa’-ul-Afhaam”, uk. 263, kupitia kwa Ja´far bin ´Awn, kutoka kwa Zakariyyaa. Kwa hiyo Athar ikathibiti namna hiyo – na himdi zote njema anastahiki Allaah.
- Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Ishaaq al-Maalikiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fadhwl-us-Swalaah ´alaan-Nabiy, uk. 73
- Imechapishwa: 06/02/2024
- taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
81 – ´Aarim bin al-Fadhwl ametuhadithia: ´Abdullaah bin al-Mubaarak ametuhadithia: Zakariyyaa ametuhadithia, kutoka kwa Wahb bin al-Ajda´: Nimemsikia ´Umar bin al-Khattwaab akisema:
”Mnapofika, basi tufuni kwenye Ka´bah mara saba na swalini Mahali pa kusimama Rak´ah mbili. Kisha nendeni Swafaa na simameni pale mnapoweza kuiona Nyumba. Pigeni Takbiyr saba. Baina ya kila Takbiyr kuna himdi na sifa kwa Allaah, kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kujiomba du´aa mwenyewe. Fanya mfano wa hivo Marwah.”[1]
[1] Cheni ya wapokezi ni Swahiyh. ´Aarim, ambaye jina lake ni Muhammad bin al-Fadhwl (´Aarim ilikuwa ni jina lake la utani), ameihifadhi. Kumbukumbu yake ilibadilika muda ulivyoenda. Wapokezi wake wengine waliobaki ni waaminifu. Ibn-ul-Qayyim ameitaja katika “Jalaa’-ul-Afhaam”, uk. 263, kupitia kwa Ja´far bin ´Awn, kutoka kwa Zakariyyaa. Kwa hiyo Athar ikathibiti namna hiyo – na himdi zote njema anastahiki Allaah.
Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Ishaaq al-Maalikiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fadhwl-us-Swalaah ´alaan-Nabiy, uk. 73
Imechapishwa: 06/02/2024
taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/81-athar-mnapofika-basi-tufuni-kwenye-kabah-mara-saba/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)