75. Maswahabah waliwapiga vita waliosema kuwa ´Aliy ni mungu

Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:

Akisema: “Walisema: “Musaylamah ni Mtume”, mwambie: “Hili ndilo lililokuwa linatakikana. Ikiwa yule anayempandisha mtu katika daraja ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anakufuru na mali yake inakuwa halali na kumwagwa damu yake, na wala shahaadah mbili na wala swalah havimfai kitu, vipi kwa mwenye kumpandisha Shamsaan, Yuusuf, Swahabah au Mtume katika daraja ya al-Jabbaar wa mbingu na ardhi? Ametakasika Allaah! Ni Ukubwa ulioje alionao:

كَذَٰلِكَ يَطْبَعُ اللَّـهُ عَلَىٰ قُلُوبِ الَّذِينَ لَا يَعْلَمُونَ

“Hivyo ndivyo Allaah anavyopiga chapa juu ya nyoyo za wale wasiojua.” (30:59)

MAELEZO

Hili ni jibu la nne. Watu hawa walikuwa wakidai Uislamu na walisoma kwa Maswahabah. Pamoja na hivyo hili halikuwazuia kuwahukumu ukafiri na kuwachoma moto pindi waliposema kuwa ´Aliy bin Abiy Twaalib ni mungu. Hayo hayo ndio yanayodaiwa na wale wenye kumuabudu Shamsaan na wengineo.

Ni vipi Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) waliafikiana kuwapiga vita watu hawa? Mnafikiria kuwa Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) wanaafikiana juu ya kumpiga vita mtu ambaye hastahiki kupigwa vita? Mnadhania kwamba wanaafikiana juu ya kumkufurisha mtu ikiwa hastahiki hilo? Ni jambo lisilowezekana. Mnafikiria kuwa na imani kwa Taaj ni jambo lisilodhuru tofauti na kwa ´Aliy bin Abiy Twaalib?

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 85-86
  • Imechapishwa: 25/11/2023