73. Matamshi ya Tashahhud – Tamko la Ibn ´Abbaas

2- Tashahhud ya Ibn ´Abbaas. Ibn ´Abbaas amesema:

“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akitufunza Tashahhud kama anavyotufunza [Suurah katika] Qur-aan: Alikuwa akisema:

التحيات المباركات الصلوات الطيبات لله، [ال]سلام عليك أيها النبي و رحمة الله و بركاته، [ال]سلام علينا و على عباد الله الصالحين، أشهد أن لا إله إلا الله و [أشهد]أن محمداً رسول الله

“Maadhimisho, baraka, swalah na mazuri yote yanamstahikia Allaah[1]. Amani, rehema na baraka za Allaah ziwe juu yako, ee Mtume! Amani ishuke juu yetu na juu ya waja wema wa Allaah. Nashuhudia ya kwamba hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah na [nashuhudia] ya kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah.”

Katika upokezi mwingine imekuja:

و أن محمداً عبده و رسوله

“… na kwamba Muhammad ni mja na Mtume Wake.”[2]

[1] an-Nawawiy amesema: ”Hadiyth inafahamisha kwamba maadhimisho na yote yaliyo baada yake yanamstahikia Allaah (Ta´ala) pekee na si mwengine.”

[2] Muslim, Abu ´Awaanah, ash-Shaafi´iy na an-Nasaa’iy.

  • Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 141
  • Imechapishwa: 30/12/2018