Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah) amesema:
Kumpiga mawe mzinifu aliyeoa/kuolewa au aliwahi kuoa/kuolewa ni haki endapo atakiri mwenyewe au kukawepo ushahidi. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipiga mawe na wale viongozi waongofu pia walipiga mawe.
MAELEZO
Hii ndio ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah inapokuja katika kumsimamishia adhabu mzinzi ambaye kishawahi kuingia katika ndoa. Anatakiwa kutekelezewa Shari´ah ya Allaah takasifu na hukumu Zake zilizoshinda. Mtu kama huyo anapaswa kupigwa mawe hadi afariki baada ya kuhukumiwa hivo na yule hakimu wa Kishari´ah ambaye kateuliwa na mtawala wa waislamu. Mkusudiwa ni yule mtu ambaye amewahi kuingia ndani ya ndoa sahihi; huyu ndiye ambaye atapigwa mawe hadharani hadi kufa. Kuna matarajio Allaah akamsamehe dhambi yake na kumwingiza Peponi.
- Muhusika: ´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Latwiyfah ´alaa Usuwl-is-Sunnah al-Muniyfah, uk. 146
- Imechapishwa: 23/06/2026
Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah) amesema:
Kumpiga mawe mzinifu aliyeoa/kuolewa au aliwahi kuoa/kuolewa ni haki endapo atakiri mwenyewe au kukawepo ushahidi. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipiga mawe na wale viongozi waongofu pia walipiga mawe.
MAELEZO
Hii ndio ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah inapokuja katika kumsimamishia adhabu mzinzi ambaye kishawahi kuingia katika ndoa. Anatakiwa kutekelezewa Shari´ah ya Allaah takasifu na hukumu Zake zilizoshinda. Mtu kama huyo anapaswa kupigwa mawe hadi afariki baada ya kuhukumiwa hivo na yule hakimu wa Kishari´ah ambaye kateuliwa na mtawala wa waislamu. Mkusudiwa ni yule mtu ambaye amewahi kuingia ndani ya ndoa sahihi; huyu ndiye ambaye atapigwa mawe hadharani hadi kufa. Kuna matarajio Allaah akamsamehe dhambi yake na kumwingiza Peponi.
Muhusika: ´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Latwiyfah ´alaa Usuwl-is-Sunnah al-Muniyfah, uk. 146
Imechapishwa: 23/06/2026
https://firqatunnajia.com/65-mamlaka-pekee-ndio-yanayotekeleza-adhabu/