60. Mwanamke mweusi wa kifafa ataingia Peponi

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimthibitishia yule mwanamke mweusi ambaye alikuwa na maradhi ya kifafa. ´Atwaa´ bin Rabaah amesimulia kuwa Ibn ´Abbaas alimwambia:

”Je, nisikuonyeshe mwanamke wa Peponi?” Nikasema: ”Ndio.” Akasema: ”Mwanamke huyu mweusi. Alimjia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: ”Mimi naugua kifafa na kubaki wazi. Niombee du´aa kwa Allaah.” Akasema: ”Ukipenda kuwa na subira na uko na Pepo, na ukitaka nitakuombea kwa Allaah akuponye.” Akasema: ”Nasubiri. Lakini nabaki wazi. Niombee kwa Allaah nisibaki wazi.” Akamuombea du´aa.”[1]

[1] al-Bukhaariy (5652), Muslim (2576) na Ahmad (3240).

  • Muhusika: ´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Latwiyfah ´alaa Usuwl-is-Sunnah al-Muniyfah, uk. 139
  • Imechapishwa: 21/05/2026