5 – Imaam al-Baghawiy amesema:

“Mu’tazilah wanafasiri Kulingana juu kwamba ni kutawala wakati Ahl-us-Sunnah wanasema kuwa Kulingana juu ya ´Arshi ni sifa ya Allaah (Ta’ala) ambayo haitakiwi kufanyiwa namna. Ni wajibu kwa mtu kuiamini na amwachie ujuzi Wake Allaah ( ́Azza wa Jall). Kuna bwana mmoja alimuuliza Maalik bin Anas kuhusu maneno Yake:

الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ

”Mwingi wa rehema amelingana juu ya ´Arshi.”[1]

”Amelingana juu vipi?” Maalik akainamisha kichwa chake kwa muda mrefu na akaanza kutokwa na jasho. Kisha akasema: “Kulingana juu si kitu kisichofahamika. Namna haifahamiki. Ni wajibu kuamini jambo hilo na kuuliza juu yake ni Bid´ah.” Mimi sikufikirii vyengine isipokuwa mpotevu.” Kisha akaamuru atolewe nje.”

Imepokewa kwamba Sufyaan ath-Thawriy, al-Awzaa’iy, al-Layth bin Sa’d, Sufyaan bin ´Uyaynah, ´Abdullaah bin al-Mubaarak na wanazuoni wengineo wa Ahl-us-Sunnah wamesema kuhusu Aayah hizi za sifa zisizo wazi:

”Zipitisheni kama zilivyokuja bila ya kuzifanyia namna.”[2]

[1] 20:05

[2] Ma´aalim-ut-Tanziyl (2/165).

  • Muhusika: Shaykh ´Abdur-Razzaaq bin ´Allaamah ´Abdil-Muhsin al-´Abbaad al-Badr
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Athar al-Mash-huur ´an-il-Imaam Maalik fiy Swifat-il-Istiwaa’, uk. 81-82
  • Imechapishwa: 17/12/2025