58. Bilaal bin Rabaah ataingia Peponi

Bilaal bin Rabaah (Radhiya Allaahu ´anh) pia ameahidiwa kuingia Peponi. Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

“Wakati wa swalah ya Fajr Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwambia Bilaal: “Ee Bilaal! Hebu nieleze kitendo ulicho na matarajio nacho zaidi ulichofanya katika Uislamu. Kwani hakika mimi nimemsikia nyayo za miguu yako Peponi.” Akasema: “Hakuna kitendo nilichofanya ambacho nina matarajio nacho zaidi kama mimi sijapatapo kujitwahirisha, pasi na kujali ni wakati wa usiku au mchana, isipokuwa nitaswali kwa twahara hiyo yale niliyoandikiwa kuswali.”[1]

[1] al-Bukhaariy (1149) na Muslim (2458).

  • Muhusika: ´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Latwiyfah ´alaa Usuwl-is-Sunnah al-Muniyfah, uk. 137-138
  • Imechapishwa: 20/05/2026