Swali: Je, du´aa ya kufungulia swalah inasomwa katika kila Rak´ah ya Tarawiyh? Kipi unachowanasihi wale maimamu wanaotosheka kusoma Tashahhud ya kwanza peke yake katika Tarawiyh?
Jibu: Tarawiyh inazingatiwa kuwa swalah moja. Tukiianza swalah kwa du´aa ya kufungulia swalah baada ya Takbiyr, basi tunatosheka nayo katika Rak´ah zilizobaki. Ni kama ambavo sisi katika swalah ya faradhi tunatosheka na du´aa ya kufungulia swalah inayosomwa katika ile Rak´ah ya kwanza.
Imewekwa katika Shari´ah kwa imamu kukamilisha Tashahhud ya mwisho. Kuomba du´aa ndani ya swalah ndio bora kuliko kuomba du´aa nje yake, kwa sababu ndani ya swalah tuko katika ´ibaadah na utiifu. Kwa ajili hiyo hatutakiwi kufanya haraka sana kiasi cha kwamba tukaacha yale mambo mengi yaliyopendekezwa. Bali tunatakiwa tuswali kwa utaratibu na tukakamilishe yale mambo yaliyopendekezwa.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aalush-Shaykh
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Min Fataawaas-Swiyaam, uk. 41-42
- Imechapishwa: 07/04/2022
Swali: Je, du´aa ya kufungulia swalah inasomwa katika kila Rak´ah ya Tarawiyh? Kipi unachowanasihi wale maimamu wanaotosheka kusoma Tashahhud ya kwanza peke yake katika Tarawiyh?
Jibu: Tarawiyh inazingatiwa kuwa swalah moja. Tukiianza swalah kwa du´aa ya kufungulia swalah baada ya Takbiyr, basi tunatosheka nayo katika Rak´ah zilizobaki. Ni kama ambavo sisi katika swalah ya faradhi tunatosheka na du´aa ya kufungulia swalah inayosomwa katika ile Rak´ah ya kwanza.
Imewekwa katika Shari´ah kwa imamu kukamilisha Tashahhud ya mwisho. Kuomba du´aa ndani ya swalah ndio bora kuliko kuomba du´aa nje yake, kwa sababu ndani ya swalah tuko katika ´ibaadah na utiifu. Kwa ajili hiyo hatutakiwi kufanya haraka sana kiasi cha kwamba tukaacha yale mambo mengi yaliyopendekezwa. Bali tunatakiwa tuswali kwa utaratibu na tukakamilishe yale mambo yaliyopendekezwa.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aalush-Shaykh
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Min Fataawaas-Swiyaam, uk. 41-42
Imechapishwa: 07/04/2022
https://firqatunnajia.com/52-duaa-ya-kufungulia-swalah-inasomwa-katika-kila-rakah-kwenye-tarawiyh/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)