Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Mwambie: “Ikiwa umekubaliana na mimi ya kwamba ni ´ibaadah na unamuomba Allaah usiku na mchana, kwa khofu na unyenyekevu, kisha ukaomba kwa haja hiyo Mtume au asiyekuwa yeye; je utakuwa umeshirikisha katika ´ibaadah ya Allaah mwengine asiyekuwa Yeye?” Hana budi kusema: “Ndio.”
MAELEZO
Baada ya kumbainishia kuwa du´aa ni ´ibaadah na akakubali, basi mwambie:
“Je, utakuwa si mwenye kumuabudu mwengine asiyekuwa Allaah endapo utatumbukia katika haja na ukamuomba Allaah (´Azza wa Jall) kisha ukamuomba Mtume au mtu mwingine haja hiyohiyo?” Hana budi kusema: “Ndio.”, ni vigumu kukwepa uhakika huu.
Haya ni kuhusiana na du´aa.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 67
- Imechapishwa: 24/11/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket