Swali 48: Ni ipi hukumu ya kuswalia kaburi wakati uliokatazwa[1]?
Jibu: Kaburi haliswaliwi wakati wa makatazo isipokuwa ikiwa hilo limetokea katika kipindi kirefu ambacho ni baada ya swalah ya ´Aswr na swalah ya Fajr. Wakati uliokatazwa hapa ni mrefu na hivyo hapana neno kuswali ndani ya wakati huu. Kwa sababu ni miongoni mwa swalah zenye sababu. Kuhusu katika wakati ambao ni mfinyu ambao ni ule wakati uliokuja katika Hadiyh ya ´Uqbah (Radhiya Allaahu ´anh) katika “as-Swahiyh” ya Muslim ambapo amesema (Radhiya Allaahu ´anh):
“Saa tatu alikuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akitukataza kuswali ndani yake na kuwazika ndani yake wafu wetu; wakati linapochomoza jua mpaka linaponyanyuka, jua linapolingamana sawasawa katikati ya mbingu mpaka lipinduke na jua linapokurubia kuzama mpaka lizame.”[2]
Haijuzu kumswalia maiti katika nyakati hizi na wala kumzika ndani yake kutokana na Hadiyth hii ambayo ni Swahiyh.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (13/156-157).
[2] Ahmad (16926) na Muslim (831).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 37-38
- Imechapishwa: 24/12/2021
Swali 48: Ni ipi hukumu ya kuswalia kaburi wakati uliokatazwa[1]?
Jibu: Kaburi haliswaliwi wakati wa makatazo isipokuwa ikiwa hilo limetokea katika kipindi kirefu ambacho ni baada ya swalah ya ´Aswr na swalah ya Fajr. Wakati uliokatazwa hapa ni mrefu na hivyo hapana neno kuswali ndani ya wakati huu. Kwa sababu ni miongoni mwa swalah zenye sababu. Kuhusu katika wakati ambao ni mfinyu ambao ni ule wakati uliokuja katika Hadiyh ya ´Uqbah (Radhiya Allaahu ´anh) katika “as-Swahiyh” ya Muslim ambapo amesema (Radhiya Allaahu ´anh):
“Saa tatu alikuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akitukataza kuswali ndani yake na kuwazika ndani yake wafu wetu; wakati linapochomoza jua mpaka linaponyanyuka, jua linapolingamana sawasawa katikati ya mbingu mpaka lipinduke na jua linapokurubia kuzama mpaka lizame.”[2]
Haijuzu kumswalia maiti katika nyakati hizi na wala kumzika ndani yake kutokana na Hadiyth hii ambayo ni Swahiyh.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (13/156-157).
[2] Ahmad (16926) na Muslim (831).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 37-38
Imechapishwa: 24/12/2021
https://firqatunnajia.com/48-kumswalia-maiti-katika-nyakati-zilizokatazwa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)