Swali: Ni ipi hukumu ya imamu anayebeba msahafu wakati wa swalah?
Jibu: Ikiwa swalah ni ya faradhi, bora ni kutofanya hivo kutokana na kule kujishughulisha katika jambo hilo. Ikiwa swalah ni ya sunnah, kitendo hicho kinafaa. Kwa sababu swalah ya faradhi inatosha baada ya “al-Faatihah” kusoma kitu chepesi. Allaah (Ta´ala) amesema:
فَاقْرَءُوا مَا تَيَسَّرَ مِنَ الْقُرْآنِ
“Basi someni kile kilicho chepesi katika Qur-aan.”[1]
Lakini katika swalah ya sunnah pengine akataka kurefusha kisomo, na khaswakhaswa pale anaposwali mwenyewe au anawaswalisha watu katika Ramadhaan na akataka kukhitimisha Qur-aan pasi na kuwatia uzito watu – katika hali hiyo hakuna neno kusoma ndani ya msahafu.
[1] 73:20
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aalush-Shaykh
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Min Fataawaas-Swiyaam, uk. 39
- Imechapishwa: 02/04/2022
Swali: Ni ipi hukumu ya imamu anayebeba msahafu wakati wa swalah?
Jibu: Ikiwa swalah ni ya faradhi, bora ni kutofanya hivo kutokana na kule kujishughulisha katika jambo hilo. Ikiwa swalah ni ya sunnah, kitendo hicho kinafaa. Kwa sababu swalah ya faradhi inatosha baada ya “al-Faatihah” kusoma kitu chepesi. Allaah (Ta´ala) amesema:
فَاقْرَءُوا مَا تَيَسَّرَ مِنَ الْقُرْآنِ
“Basi someni kile kilicho chepesi katika Qur-aan.”[1]
Lakini katika swalah ya sunnah pengine akataka kurefusha kisomo, na khaswakhaswa pale anaposwali mwenyewe au anawaswalisha watu katika Ramadhaan na akataka kukhitimisha Qur-aan pasi na kuwatia uzito watu – katika hali hiyo hakuna neno kusoma ndani ya msahafu.
[1] 73:20
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aalush-Shaykh
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Min Fataawaas-Swiyaam, uk. 39
Imechapishwa: 02/04/2022
https://firqatunnajia.com/48-imamu-anabeba-msahafu-ndani-ya-swalah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)