Ahl-ul-Hadiyth wanaharamisha ulevi uliyotengenezwa na zabibu, tende, asali, mahindi au kitu kingine kinacholevya. Wanaharamisha kiwango chake kidogo na kiwango chake kikubwa. Wanajiepusha nayo, wanaizingatiwa kuwa ni najisi na wanaona adhabu juu yake.
Wanaona kufanya haraka kutekeleza swalah. Kwa ajili ya kutaraji kupata thawabu nzuri wanaona bora ni kuiswali mwanzoni mwa wakati kuliko kuichelewesha mwishoni mwa wakati wake.
Wanaona kuwa ni wajibu kusoma al-Faatihah nyuma ya imamu.
Wanaamrisha kukamilisha Rukuu´ na Sujuud na kuzingatia ukamilishwaji wake kuwa ni jambo la wajibu. Wanaona kuwa kukamilisha Rukuu´ na Sujuud kwa kutulia, kuinuka kutoka katika Rukuu´, kunyooka sawasawa na kutulia wakati wa kuinuka kutoka kwenye Rukuu´ na pia kutulia wakati wa kutoka kwenye Sujuud na kukaa kati ya Sujuud mbili hali ya utulivu kwamba ni katika nguzo za swalah. Swalah haisihi isipokuwa kwa mambo hayo.
- Mhusika: Imaam Abu ´Uthmaan Ismaa´iyl bin ´Abdir-Rahmaan as-Swaabuuniy (afk. 449)
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ´Aqiydat-us-Salaf wa Aswhaab-il-Hadiyth, uk. 297-298
- Imechapishwa: 26/12/2023
Ahl-ul-Hadiyth wanaharamisha ulevi uliyotengenezwa na zabibu, tende, asali, mahindi au kitu kingine kinacholevya. Wanaharamisha kiwango chake kidogo na kiwango chake kikubwa. Wanajiepusha nayo, wanaizingatiwa kuwa ni najisi na wanaona adhabu juu yake.
Wanaona kufanya haraka kutekeleza swalah. Kwa ajili ya kutaraji kupata thawabu nzuri wanaona bora ni kuiswali mwanzoni mwa wakati kuliko kuichelewesha mwishoni mwa wakati wake.
Wanaona kuwa ni wajibu kusoma al-Faatihah nyuma ya imamu.
Wanaamrisha kukamilisha Rukuu´ na Sujuud na kuzingatia ukamilishwaji wake kuwa ni jambo la wajibu. Wanaona kuwa kukamilisha Rukuu´ na Sujuud kwa kutulia, kuinuka kutoka katika Rukuu´, kunyooka sawasawa na kutulia wakati wa kuinuka kutoka kwenye Rukuu´ na pia kutulia wakati wa kutoka kwenye Sujuud na kukaa kati ya Sujuud mbili hali ya utulivu kwamba ni katika nguzo za swalah. Swalah haisihi isipokuwa kwa mambo hayo.
Mhusika: Imaam Abu ´Uthmaan Ismaa´iyl bin ´Abdir-Rahmaan as-Swaabuuniy (afk. 449)
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: ´Aqiydat-us-Salaf wa Aswhaab-il-Hadiyth, uk. 297-298
Imechapishwa: 26/12/2023
https://firqatunnajia.com/45-maadili-mema-ya-ahl-us-sunnah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)