5 – Kichenguzi cha swawm aina ya tano ni kujitapisha. Maana yake ni kutoa kilichomo tumboni, chakula au kinywaji, kwa njia ya mdomo kwa kukusudia. Hii ni kwa maneno (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
”Ambaye atajitapisha basi ni lazima kwake kulipa.”[1]
Ni nzuri kwa mujibu wa at-Tirmidhiy.
Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema:
”Akakataza (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kutoa kile kinachompa nguvu na kinachomlisha katika chakula na kinywaji ambavyo vinamtia nguvu katika mwili, kwa sababu kukitoa kunasababisha kupungua kwa nguvu na kudhoofika kwa mwili. Akiruhusiwa kufanya hivyo hujidhuru na huwa amepitiliza katika ´ibaadah yake bila kuwa na uadilifu ndani yake.
Ama ikiwa matapishi yamemshinda na yakatoka bila kutaka kwake, basi hilo halina athari juu ya swawm yake. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
”Ambaye yatamshinda matapishi basi halazimiki kulipa.”[2]
[1] at-Tirmidhiy (720), Abu Daawuud (2380) na Ibn Maajah (1676). Abu ´Iysaa amesema:
”Hadiyth ni nzuri na ngeni.”
Amesema tena:
”Imefanyiwa kazi na wanazuoni.”
[2] at-Tirmidhiy (720), Abu Daawuud (2380) na Ibn Maajah (1676). Abu ´Iysaa amesema:
”Hadiyth ni nzuri na ngeni.”
Amesema tena:
”Imefanyiwa kazi na wanazuoni.”
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ithaaf Ahl-il-Iymaan bi Duruus Shahri Ramadhwaan, uk. 42-43
- Imechapishwa: 14/03/2026
5 – Kichenguzi cha swawm aina ya tano ni kujitapisha. Maana yake ni kutoa kilichomo tumboni, chakula au kinywaji, kwa njia ya mdomo kwa kukusudia. Hii ni kwa maneno (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
”Ambaye atajitapisha basi ni lazima kwake kulipa.”[1]
Ni nzuri kwa mujibu wa at-Tirmidhiy.
Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema:
”Akakataza (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kutoa kile kinachompa nguvu na kinachomlisha katika chakula na kinywaji ambavyo vinamtia nguvu katika mwili, kwa sababu kukitoa kunasababisha kupungua kwa nguvu na kudhoofika kwa mwili. Akiruhusiwa kufanya hivyo hujidhuru na huwa amepitiliza katika ´ibaadah yake bila kuwa na uadilifu ndani yake.
Ama ikiwa matapishi yamemshinda na yakatoka bila kutaka kwake, basi hilo halina athari juu ya swawm yake. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
”Ambaye yatamshinda matapishi basi halazimiki kulipa.”[2]
[1] at-Tirmidhiy (720), Abu Daawuud (2380) na Ibn Maajah (1676). Abu ´Iysaa amesema:
”Hadiyth ni nzuri na ngeni.”
Amesema tena:
”Imefanyiwa kazi na wanazuoni.”
[2] at-Tirmidhiy (720), Abu Daawuud (2380) na Ibn Maajah (1676). Abu ´Iysaa amesema:
”Hadiyth ni nzuri na ngeni.”
Amesema tena:
”Imefanyiwa kazi na wanazuoni.”
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ithaaf Ahl-il-Iymaan bi Duruus Shahri Ramadhwaan, uk. 42-43
Imechapishwa: 14/03/2026
https://firqatunnajia.com/43-kujitapisha-kunamfunguza-mfungaji/