4. Na yeyote anayetaka dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitokubaliwa kutoka kwake

Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Matendo yatakuja siku ya Qiyaamah. Swalah itakuja na iseme: “Ee Mola! Mimi ndio swalah.” Aseme: “Uko katika kheri.” Kisha ije swadaqah na iseme: “Ee Mola! Mimi ndio swadaqah.” Aseme: “Uko katika kheri.” Kisha ije swawm na isema: “Ee Mola! Mimi ndio swawm.” Aseme: “Uko katika kheri.” Halafu yaje matendo mengine yote na aseme: “Uko katika kheri.” Halafu kuje Uislamu na usema: “Ee Mola! Wewe ni as-Salaam na mimi ndio Uislamu.” Aseme: “Uko katika kheri.” Leo hii nitachukua na kupeana kutokana na wewe.” Allaah (Ta´ala) amesema:

وَمَن يَبْتَغِ غَيْرَ الْإِسْلَامِ دِينًا فَلَن يُقْبَلَ مِنْهُ وَهُوَ فِي الْآخِرَةِ مِنَ الْخَاسِرِينَ

“Na yeyote anayetaka dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitokubaliwa kutoka kwake, naye katika Aakhirah atakuwa miongoni mwa waliokhasirika.” (03:85)

Ameipokea Ahmad.

Kumepokelewa [Hadiyth] Swahiyh ya kwamba ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ameeleza kuwa Mtume wa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Yule mwenye kufanya tendo lisiloafikiana na amri yetu litarudishwa.”

  • Mhusika: Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwl-ul-Islaam, uk. 16-17
  • Imechapishwa: 23/10/2016