38. Kupitiwa na usingizi na kukosa kisomo cha usiku

´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mwenye kulala akakosa sehemu yake ya usiku au sehemu yake, kisha akaisoma kati ya swalah ya Fajr na swalah ya Dhuhr, basi ataandikiwa kama kwamba aliisoma usiku.”[1]

Ameipokea Muslim.

Sulaymaan bin Yasaar ameeleza ya kwamba Abu Usayd (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

”Nililala jana usiku nikakosa sehemu yangu ya kusoma mpaka nikafika asubuhi. Nilipoamka nilisema:

إِنَّا لِلّهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعونَ

”Hakika sisi ni wa Allaah na hakika Kwake tutarejea.”

Sehemu yangu ilikuwa ni Suurah al-Baqarah. Nikamuona katika ndoto kama kwamba ng’ombe ananipiga kwa pembe.”

Ameipokea Ibn Abiy Daawuud.

Ibn Abiyd-Dunyaa ameeleza:

”Bwana mmoja, ambaye alikuwa amehifadhi Qur-aan, alilala usiku mmoja ambapo akakosa sehemu yake, basi akaoneshwa katika ndoto yake kama kwamba kuna msemaji anayemwambia:

Ninashangaa kwa mwili na afya

na kijana aliyelala mpaka alfajiri

Na kifo hakiaminiki ghafla zake

Katika giza la usiku kinapopita.

[1] Muslim (747), Abu Daawuud (1313), at-Tirmidhiy (581), an-Nasaa’iy (1791-1792) na Ibn Maajah (1343).

  • Muhusika: Imaam Yahyaa bin Sharaf an-Nawawiy (afk. 677)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tibyaan fiy Aadaabi Hamalat-il-Qur-aan, uk. 48
  • Imechapishwa: 26/08/2026