Imethibiti kutoka kwa Abu Muusaa al-Ash´ariy (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Iangalieni hii Qur-aan! Naapa kwa Yule ambaye nafsi ya Muhammad iko mkononi Mwake, hakika ni yenye kutoroka zaidi kuliko ngamia walioko katika kamba zao.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mfano wa mwenye Qur-aan ni kama mfano wa ngamia waliofungwa; akiwatunza anawashikilia, na akiwaachia wanaondoka.”[2]
Ameipokea Muslim na al-Bukhaariy.
Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Zilioneshwa kwangu thawabu za ummah wangu, hata uchafu mdogo anaoutoa mtu msikitini, na zilioneshwa kwangu dhambi za ummah wangu, basi sikuona dhambi kubwa zaidi kuliko Suurah katika Qur-aan au Aayah aliyopewa mtu kisha akaisahau.”[3]
Ameipokea Abu Daawuud na at-Tirmidhiy. Hata hivyo imetiwa dosari.
Sa´d bin ´Ubaadah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza ya kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kusoma Qur-aan kisha akaisahau atakutana na Allaah (´Azza wa Jall) siku ya Qiyaamah hali ya kuwa amekatwa mkono.”[4]
Ameipokea Abu Daawuud na at-Tirmidhiy.
[1] al-Bukhaariy (5033) na Muslim (791).
[2] al-Bukhaariy (5031) na Muslim (789).
[3] Abu Daawuud (461) na at-Tirmidhiy (2916). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Dhwa´iyf Sunan Abiy Daawuud” (461).
[4] Abu Daawuud (1474) na ad-Daarimiy (3340). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Dhwa´iyf Sunan Abiy Daawuud” (1474).
- Muhusika: Imaam Yahyaa bin Sharaf an-Nawawiy (afk. 677)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Tibyaan fiy Aadaabi Hamalat-il-Qur-aan, uk. 45-47
- Imechapishwa: 26/08/2026
Imethibiti kutoka kwa Abu Muusaa al-Ash´ariy (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Iangalieni hii Qur-aan! Naapa kwa Yule ambaye nafsi ya Muhammad iko mkononi Mwake, hakika ni yenye kutoroka zaidi kuliko ngamia walioko katika kamba zao.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mfano wa mwenye Qur-aan ni kama mfano wa ngamia waliofungwa; akiwatunza anawashikilia, na akiwaachia wanaondoka.”[2]
Ameipokea Muslim na al-Bukhaariy.
Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Zilioneshwa kwangu thawabu za ummah wangu, hata uchafu mdogo anaoutoa mtu msikitini, na zilioneshwa kwangu dhambi za ummah wangu, basi sikuona dhambi kubwa zaidi kuliko Suurah katika Qur-aan au Aayah aliyopewa mtu kisha akaisahau.”[3]
Ameipokea Abu Daawuud na at-Tirmidhiy. Hata hivyo imetiwa dosari.
Sa´d bin ´Ubaadah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza ya kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kusoma Qur-aan kisha akaisahau atakutana na Allaah (´Azza wa Jall) siku ya Qiyaamah hali ya kuwa amekatwa mkono.”[4]
Ameipokea Abu Daawuud na at-Tirmidhiy.
[1] al-Bukhaariy (5033) na Muslim (791).
[2] al-Bukhaariy (5031) na Muslim (789).
[3] Abu Daawuud (461) na at-Tirmidhiy (2916). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Dhwa´iyf Sunan Abiy Daawuud” (461).
[4] Abu Daawuud (1474) na ad-Daarimiy (3340). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Dhwa´iyf Sunan Abiy Daawuud” (1474).
Muhusika: Imaam Yahyaa bin Sharaf an-Nawawiy (afk. 677)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Tibyaan fiy Aadaabi Hamalat-il-Qur-aan, uk. 45-47
Imechapishwa: 26/08/2026
https://firqatunnajia.com/37-ichunge-qur-aan-na-usiisahau/