Miongoni mwa ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni kwamba Allaah ameyataka matendo yote ya waja, ni mamoja matendo yake ya kheri na matendo yake ya shari. Hakuna mtu yeyote aliyeamini isipokuwa kwa matakwa Yake na hakuna yeyote aliyekufuru isipokuwa kwa utashi Wake. Iwapo angelitaka basi angeliwafanya watu wote kuwa ummah mmoja. Angelitaka asiasiwe basi asingemuumba Ibliys. Kukufuru kwa makafiri na kuamini kwa waumini ni kwa mipango, makadirio, matakwa na utashi Wake. Ameyataka yote hayo na kuyakadiria. Anaridhika kwa imani na utiifu na anakasirishwa kwa kufuru na maasi. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
إِن تَكْفُرُوا فَإِنَّ اللَّـهَ غَنِيٌّ عَنكُمْ ۖ وَلَا يَرْضَىٰ لِعِبَادِهِ الْكُفْرَ
“Mkikufuru, basi hakika Allaah ni mkwasi kwenu, na wala haridhii kwa waja Wake ukafiri.”[1]
[1] 39:7
- Mhusika: Imaam Abu ´Uthmaan Ismaa´iyl bin ´Abdir-Rahmaan as-Swaabuuniy (afk. 449)
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ´Aqiydat-us-Salaf wa Aswhaab-il-Hadiyth, uk. 285-286
- Imechapishwa: 20/12/2023
Miongoni mwa ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni kwamba Allaah ameyataka matendo yote ya waja, ni mamoja matendo yake ya kheri na matendo yake ya shari. Hakuna mtu yeyote aliyeamini isipokuwa kwa matakwa Yake na hakuna yeyote aliyekufuru isipokuwa kwa utashi Wake. Iwapo angelitaka basi angeliwafanya watu wote kuwa ummah mmoja. Angelitaka asiasiwe basi asingemuumba Ibliys. Kukufuru kwa makafiri na kuamini kwa waumini ni kwa mipango, makadirio, matakwa na utashi Wake. Ameyataka yote hayo na kuyakadiria. Anaridhika kwa imani na utiifu na anakasirishwa kwa kufuru na maasi. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
إِن تَكْفُرُوا فَإِنَّ اللَّـهَ غَنِيٌّ عَنكُمْ ۖ وَلَا يَرْضَىٰ لِعِبَادِهِ الْكُفْرَ
“Mkikufuru, basi hakika Allaah ni mkwasi kwenu, na wala haridhii kwa waja Wake ukafiri.”[1]
[1] 39:7
Mhusika: Imaam Abu ´Uthmaan Ismaa´iyl bin ´Abdir-Rahmaan as-Swaabuuniy (afk. 449)
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: ´Aqiydat-us-Salaf wa Aswhaab-il-Hadiyth, uk. 285-286
Imechapishwa: 20/12/2023
https://firqatunnajia.com/36-yote-yanatokea-kwa-utashi-wa-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)