20 – Kuwaombea mabaya watoto:

Miongoni mwa makosa yanayoenda kinyume na Shari´ah ni kuwaombea mabaya watoto. Kwa kosa dogo tu utamuona mama anainua mikono na kutoa laana dhidi ya watoto wake. Waombee du´aa njema badala ya kuwaombea mabaya na jizoweze kufanya hivyo. Hili ni muhimu, kwani du´aa inaweza kukutana wakati wa kukubaliwa du´aa na baadaye ukajutia na majuto ni mjukuu. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Msijiombee mabaya wala msiwaombee mabaya watoto wenu …”

Ameipokea Muslim.

  • Muhusika: Dr. ´Abdul-´Aziyz bin Daawuud al-Faaiz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Tawjiyhaat wa Tanbiyhaat lil-Fataati al-Muslimah, uk. 32
  • Imechapishwa: 19/03/2026