Bali kiumbe si muweza wa kuelewa namna vilivyo viumbe vingi. Kwa hivyo anakuwa na haki zaidi ya kushindwa kuelewa uhalisia na namna zilivyo sifa za Muumba.  Rustah amesema:

“Nilimsikia Ibn Mahdiy akimwambia mmoja kutoka katika kizazi cha wanamfalme wa Ja’far bin Sulaymaan: “Nimefikiwa na khabari kwamba unazungumza juu ya Mola, ukimuelezea Yeye na kumfananisha.” Akasema: “Ndio. Tumetafakari na kuona kuwa hakuna chochote katika viumbe vya Allaah kilicho bora kama mwanadamu.” Hivo akaanza kuzungumza juu ya sifa na urefu, kisha akamwambia: “Tulia, ee mwanangu! Hebu kwanza tuzungumze kidogo juu ya kiumbe. Ikiwa tutashindwa kuzungumza juu yake, basi kwa Muumba ndio hatuwezi hata kidogo. Nisimulie yale aliyokuhadithia Shu’bah, kutoka kwa Ash-Shaybaaniy, kutoka kwa Sa’iyd bin Jubayr, kutoka kwa ´Abdullaah, ambaye amesema kuhusiana na maneno Yake (Ta’ala):

لَقَدْ رَأَىٰ مِنْ آيَاتِ رَبِّهِ الْكُبْرَىٰ

“Hakika aliona miongoni mwa alama za Mola wake kubwa kabisa.”[1]

“Alimuona Jibriyl akiwa na mbawa mia sita.”

Mvulana akabaki mwenye kukodoa macho. Akasema: “Acha nikufanyie wepesi; nieleze kiumbe mwenye mbawa tatu na uweke bawa la tatu mahali pake ili nipate kujua.” Ndipo akasema: “Ee Abu Sa’iyd! Tumeshindwa kumweleza kiumbe. Nakushuhudisha kwmaba nimeshindwa na hivyo akajirejea maoni yake.”[2]

[1] 53:18

[2] al-Laalakaa’iy (3/530) na Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (9/196-197), ambaye tamko ni lake.

  • Muhusika: Shaykh ´Abdur-Razzaaq bin ´Allaamah ´Abdil-Muhsin al-´Abbaad al-Badr
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Athar al-Mash-huur ´an-il-Imaam Maalik fiy Swifat-il-Istiwaa’, uk. 55-56
  • Imechapishwa: 03/12/2025