Ama kuhusu wakati wa kuanza na kumaliza kwa yule anayeikhitimisha katika wiki, Ibn Abiy Daawuud amepokea kwamba ´Uthmaan bin ´Affaan (Radhiya Allaahu ´anh) alikuwa anaanza kuisoma Qur-aan usiku wa ijumaa na kuimaliza usiku wa alkhamisi. Imaam Abu Haamid al-Ghazaaliy (Rahimahu Allaah) amesema katika ”al-Ihyaa”:

”Lililo bora ni kuisoma yote mara moja usiku na nyingine mchana; afanye hitimisho moja ya mchana siku ya jumatatu katika Rak´ah mbili za Fajr au baada yake, na afanye hitimisho nyingine usiku wa ijumaa katika Rak´ah mbili za Maghrib au baada yake, ili aupokee mwanzo wa mchana na mwisho wake.”

Ibn Abiy Daawuud amepokea kutoka kwa mwanafunzi wa Maswahabah ´Umar bin Murrah, ambaye amesema:

”Walikuwa wanapenda kuisoma Qur-aan yote mwanzoni mwa usiku au mwanzoni mwa mchana.”

Mwanafunzi mtukufu wa Maswahabah Twalhah bin Muswarrif amesema:

”Mwenye kuisoma Qur-aan yote wakati wowote wa mchana, basi Malaika humswalia mpaka jioni. Na wakati wowote wa usiku, basi Malaika humswalia mpaka kupambazuke asubuhi.”

Mujaahid amesema mfano wa hayo. ad-Daarimiy amepokea kwamba Sa´d bin Abiy Waqqaas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

”Ikiwa usomaji wote wa Qur-aan utakutana na mwanzo wa usiku, basi Malaika humswalia mpaka kupambazuke asubuhi. Na ikiwa utakutana na mwisho wa usiku, basi Malaika humswalia mpaka kuingie jioni.”[1]

ad-Daarimiy amesema:

”Hii ni nzuri kutoka kwa Sa´d.”

Mwanafunzi wa Maswahabah Habiyb bin Abiy Thaabit alikuwa akiisoma Qur-aan yote kabla ya kwenda katika Rukuu´. Ibn Abiy Daawuud amesema:

”Vivyo hivyo amesema Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah).”

Sehemu nyingine ya mlango huu itayokuja huko mbele – Allaah akitaka.

[1] ad-Daarimiy (3482).

  • Muhusika: Imaam Yahyaa bin Sharaf an-Nawawiy (afk. 677)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tibyaan fiy Aadaabi Hamalat-il-Qur-aan, uk. 42
  • Imechapishwa: 26/08/2026