167- Kukusudia kwenda kutembea Yerusalemu baada ya kuhiji na kusema:
قدس الله حجتك
“Allaah aitakase hajj yako.”
168- Kutufu kwenye msikiti wa mwamba kama ambavyo watu wanavyotufu kwenye Ka´bah.
169- Kuadhimisha mwamba kwa aina yoyote ile ya maadhimisho. Kwa mfano kulipapasapapasa, kulibusu, kuwapeleka kondoo hapo ili kuwachinjia hapo, kujenga juu yake na mfano wake.
170- Kuna ambao wanadai kwamba kwenye mwamba mtu anaweza kuona athari ya miguu ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na athari ya kilemba chake. Wako ambao wanadhani kwamba ndio mahali ambapo Allaah (Subhanaahu wa Ta´ala) anaweka mguu Wake.
171- Kutembelea sehemu ambayo wanadai ndiko kazaliwa ´Iysaa (´alayhis-Salaam).
172- Wanadai kwamba huko ndiko kuna Njia na Mizani. Wanasema pia kwamba njia itayotofautisha baina ya Pepo na Moto ni ukuta huo uliojengwa mashariki mwa msikiti.
173- Kuadhimisha mnyororo na sehemu zake.
174- Kuswali kwenye kaburi la Ibraahiym (´alayhis-Salaam).
175- Kukusanyika katika msimu wa hajj katika msikiti wa Aqswaa´ ili kuimba nyimbo na kupiga dufu.
Haya ndio ya mwisho niliyoweza kukusanya katika Bid´ah za hajj na matembezi yake. Ninamuomba Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) ayajaalie kuwa ni yenye kuwasaidia waislamu juu ya kumuiga bwana wa Mitume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Kutakasika kutokamana na mapungufu ni Kwako, ee Allaah, na himdi zote ni Zako. Nashuhudia ya kwamba hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah. Nakuomba msamaha na kutubia Kwako.
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Manaasik-ul-Hajj wal-´Umrah, uk. 60-61
- Imechapishwa: 22/07/2018
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)