Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah) amesema:
“Yule mwenye kuacha swalah amekufuru. Hakuna katika matendo kitu kukiacha ni kufuru isipokuwa swalah. Mwenye kuiacha ni kafiri. Allaah amehalalisha kumuua.”
MAELEZO
Waandishi wa “as-Sunnah” wamepokea kwa cheni ya wapokezi Swahiyh ya kwamba Buraydah bin al-Haaswib (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ahadi iliopo kati yetu sisi na wao ni swalah. Hivyo basi, yule mwenye kuiacha amekufuru.”[1]
Muslim amepokea kwamba Jaabir (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kati ya mtu na ukafiri ni kuacha swalah.”[2]
Abu Waa-il bin Shaqiyq bin Salamah amesema:
“Hakuna kitu ambacho Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walikuwa wakiona kukiacha ni ukafiri isipokuwa swalah.”[3]
Hapa Ahmad anasema:
“Hakuna katika matendo kitu kukiacha ni kufuru isipokuwa swalah. Mwenye kuiacha ni kafiri. Allaah amehalalisha kumuua.”
[1] at-Tirmidhiy (2621), an-Nasaa’iy (463) na Ibn Maajah (1079). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy.
[2] at-Tirmidhiy (2619), an-Nasaa’iy (464) na Ibn Maajah (1078). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy.
[3] at-Tirmidhiy (2622). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy.
- Muhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Itmaam-ul-Minnah, uk. 131-132
- Imechapishwa: 25/04/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)