Imaam Ibn Qudaamah (Rahimahu Allaah) amesema:
Amesema (Subhaanah):
وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا
”Na atakapokuja Mola Wako na Malaika safu kwa safu.”[1]
هَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا أَن يَأْتِيَهُمُ اللَّـهُ
”Je, wanangojea nini isipokuwa Allaah awajie.”[2]
MAELEZO
4 – Ujio. Kuja kwa Allaah kwa ajili ya kutoa hukumu kati ya waja siku ya Qiyaamah kumethibiti kwa Qur-aan, Sunnah na maafikiano ya Salaf. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا
”Na atakapokuja Mola Wako na Malaika safu kwa safu.”
هَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا أَن يَأْتِيَهُمُ اللَّـهُ
”Je, wanangojea nini isipokuwa Allaah awajie.”
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“… mpaka pale watapobaki isipokuwa wale wanaomwabudu Allaah ndipo atawajia Mola wa walimwengu.”[3]
Kuna maafikiano juu yake.
Salaf wameafikiana juu ya kuthibitisha kuja kwa Allaah (Ta´ala). Kwa hiyo ni lazima kumthibitishia nayo pasi na kupotosha, kukanusha, kufanyia namna wala kupigia mfano. Ni kuja kikweli ambako kunalingana na Allaah (Ta´ala).
Ahl-ut-Ta´twiyl wameifasiri kwamba ni kuja kwa amri Yake. Tunawaraddi kwa yale yaliyokwishatangulia katika kanuni ya nne.
[1] 89: 22
[2] 02:210
[3] al-Bukhaariy (7439) na Muslim (183).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 52
- Imechapishwa: 18/10/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)