Swali 275: Ni ipi tofauti kati ya matembezi ya wanawake kulitembelea kaburi la Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na makaburi mengine? Je, makatazo ni yenye kuenea au kunabaguliwa kaburi la Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?
Jibu: Hakuna dalili inayoonyesha kuwa kaburi la Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) linatoka nje ya makatazo. Kwa ajili hiyo naona kuwa matembezi ya mwanamke kulitembelea kaburi la Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni kama kuyatembelea makaburi mengine. Inamtosha mwanamke kule kumsalimia kwake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pale anaposwali. Wakati anapomsalimia basi salamu yake inamfikia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) popote anapokuwa.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/316)
- Imechapishwa: 29/05/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket