49 – Abu ´Amr, mtumwa wa Banuu Haashim aliyeachwa huru, ametukhabarisha: Abu Haatim ar-Raaziy ametuhadithia: Abul-Yamaan ametuhadithia: Shu´ayb ametuhadithia: Abuz-Zinaad ametuhadithia, kutoka kwa al-A´raj, kutoka kwa Abu Hurayrah, ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mkono wa wa Allaah umejaa. Haupungui kwa kutoa usiku na mchana. Mnaonaje yale aliyotoa tangu aumbe mbingu na ardhi pasi na kupungua chochote kilichoko katika mkono Wake? ´Arshi Yake iko juu ya maji na kwenye mkono Wake mwingine kuna mzani ambao ndiyo anashusha na kupandisha.”[1]

[1] al-Bukhaariy (4684), Muslim (993), Ahmad (2/242) na at-Tirmidhiy (3045).

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Ishaaq bin Mandah (afk. 395)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah, uk. 76
  • Imechapishwa: 16/06/2026
  • Taaliki: ´Allaamah ´Aliy bin Naaswir al-Faqiyhiy