Swali 24: Ni ipi hukumu ya salamu baada ya Sunnah[1]?
Jibu: Ni jambo limewekwa katika Shari´ah kwa wenye kukutana katika safu mmoja akamsalimia mwengine na wakapeana mikono. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakuna waislamu wawili wanaokutana ambapo wakapeana mikono isipokuwa Allaah huwasamehe kabla hawajaachana.”[2]
Anas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walikuwa wanapokutana basi wanapeana mikono na wanapofika kutoka safarini basi wanakumbatiana.”
Vilevile imethibiti kutoka kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba amesema:
“Naapa kwa Yule ambaye nafsi yangu iko mikononi mwake hamtoingia Peponi mpaka muamini na wala hamtoamini mpaka mpendane. Je, nisikujulisheni kitu ambacho mkikifanya mtapendana; sambazeni salamu kati yenu.”[3]
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Pia aliulizwa ni Uislamu upi bora zaidi ambapo akajibu kwa kusema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kulisha chakula na kumtolea salamu unayemjua na usiyemjua.”[4]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Isipokuwa ambaye umekutana naye unajua kuwa ni kafiri. Katika hali hiyo usianze kumtolea salamu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Msianze kuwatolea salamu mayahudi wala manaswara.”[5]
Hadiyth ameipokea Muslim.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (12/411-412).
[2] at-Tirmidhiy (2651) na Abu Daawuud (4536).
[3] Muslim (81), at-Tirmidhiy (2434) na Ahmad (1355).
[4] al-Bukhaariy (11, 27) na Muslim (56).
[5] Muslim (4030) na at-Tirmidhiy (2624).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam Swalaat-il-Jumu´ah wal-Jamaa´ah, uk. 65-66
- Imechapishwa: 29/11/2021
Swali 24: Ni ipi hukumu ya salamu baada ya Sunnah[1]?
Jibu: Ni jambo limewekwa katika Shari´ah kwa wenye kukutana katika safu mmoja akamsalimia mwengine na wakapeana mikono. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakuna waislamu wawili wanaokutana ambapo wakapeana mikono isipokuwa Allaah huwasamehe kabla hawajaachana.”[2]
Anas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walikuwa wanapokutana basi wanapeana mikono na wanapofika kutoka safarini basi wanakumbatiana.”
Vilevile imethibiti kutoka kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba amesema:
“Naapa kwa Yule ambaye nafsi yangu iko mikononi mwake hamtoingia Peponi mpaka muamini na wala hamtoamini mpaka mpendane. Je, nisikujulisheni kitu ambacho mkikifanya mtapendana; sambazeni salamu kati yenu.”[3]
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Pia aliulizwa ni Uislamu upi bora zaidi ambapo akajibu kwa kusema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kulisha chakula na kumtolea salamu unayemjua na usiyemjua.”[4]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Isipokuwa ambaye umekutana naye unajua kuwa ni kafiri. Katika hali hiyo usianze kumtolea salamu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Msianze kuwatolea salamu mayahudi wala manaswara.”[5]
Hadiyth ameipokea Muslim.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (12/411-412).
[2] at-Tirmidhiy (2651) na Abu Daawuud (4536).
[3] Muslim (81), at-Tirmidhiy (2434) na Ahmad (1355).
[4] al-Bukhaariy (11, 27) na Muslim (56).
[5] Muslim (4030) na at-Tirmidhiy (2624).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ahkaam Swalaat-il-Jumu´ah wal-Jamaa´ah, uk. 65-66
Imechapishwa: 29/11/2021
https://firqatunnajia.com/24-ibn-baaz-kuhusu-kusalimiana-baada-ya-swalah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)