07 – Kusikiliza nyimbo

Miongoni mwa makosa yanayoenda kinyume na Shari´ah ni kusikiliza nyimbo, jambo ambalo ni haramu kwa dalili ya Qur-aan na Sunnah. Amesema (Ta´ala):

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَشْتَرِي لَهْوَ الْحَدِيثِ لِيُضِلَّ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَيَتَّخِذَهَا هُزُوًا ۚ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ

“Miongoni mwa watu wako ambao hununua maneno ya upuuzi ili wapoteze kutokamana na njia ya Allaah pasi na elimu na huichukulia mzaha – hao watapata adhabu ya kutweza.”[1]

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Naapa kwa Allaah kwamba watakuwepo katika ummah wangu watu ambao watahalalisha uzinzi, hariri na ala za muziki.”[2]

Nyimbo inazalisha unafiki ndani ya moyo, kama alivyopokea Imaam Ahmad. Kwa hivyo yabadilishe kwa maneno ya Allaah na kaseti za Kiislamu zenye faida na kunufaisha.

[1] 31:06

[2] al-Bukhaariy na Abu Daawuud.

  • Muhusika: Dr. ´Abdul-´Aziyz bin Daawuud al-Faaiz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Tawjiyhaat wa Tanbiyhaat lil-Fataati al-Muslimah, uk. 29
  • Imechapishwa: 17/02/2026