Shaykh-ul-Islaam na Imaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Mambo yanayochengua wudhuu´ ni manane:
1 – Kila kinachotoka kupitia tupu ya mbele au ya nyuma.
2 – Kila kichafu au najisi inayotoka kwenye mwili.
3 – Kutokwa na akili.
4 – Kumgusa mwanamke kwa matamanio.
5 – Kugusa tupu ya mbele au ya nyuma kwa mkono.
6 – Kula nyama ya ngamia.
7 – Kuosha maiti.
8 – Kuritadi kutoka katika Uislamu – Tunamuomba Allaah Atukinge na hilo.
MAELEZO
Mambo yanayochengua wudhuu´ ni yale mambo yanayoubatilisha ambapo akifanya moja wapo basi wudhuu´ wake unavunjika. Ni kama mfano wa mambo yanayochengua Uislamu kukikusudiwa yanayoubatilisha.
Manane – Mambo yanayochengua na kuvunja wudhuu´ ni manane. Mambo haya ni kwa mujibu wa madhehebu ya Hanaabilah. Mambo haya manane hakuna maafikiano juu yake.
1 – Kila kinachotoka kupitia tupu ya mbele au ya nyuma
Hichi ni kichenguzi cha kwanza miongoni mwa vichenguzi vya wudhuu´. Kinachotoka kupitia tupu ya mbele au ya nyuma ni kama mfano wa mkojo, kinyesi, manii, madhiy, wadiy na upepo. Mambo haya yanachengua wudhuu´ kwa maafikiano[1]. Kuna jopo kubwa la wanachuoni ambao hawaoni kuchenguka kwa wudhuu´ isipokuwa tu kwa kile chenye kutoka kupitia njia mbili hizi. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy (Rahimahu Allaah) katika “as-Swahiyh” yake[2] ameweka mlango ambapo akasema:
“Mlango wale wasioonelea kuchenguka kwa wudhuu´ isipokuwa kwa kile chenye kutoka kupitia tupu ya mbele na ya nyuma.”
[1] Tazama ”al-Ijmaa”, uk. 31 ya Ibn-ul-Mundhir.
[2] Kitaab-ul-Wudhuu´.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 33-35
- Imechapishwa: 16/12/2021
Shaykh-ul-Islaam na Imaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Mambo yanayochengua wudhuu´ ni manane:
1 – Kila kinachotoka kupitia tupu ya mbele au ya nyuma.
2 – Kila kichafu au najisi inayotoka kwenye mwili.
3 – Kutokwa na akili.
4 – Kumgusa mwanamke kwa matamanio.
5 – Kugusa tupu ya mbele au ya nyuma kwa mkono.
6 – Kula nyama ya ngamia.
7 – Kuosha maiti.
8 – Kuritadi kutoka katika Uislamu – Tunamuomba Allaah Atukinge na hilo.
MAELEZO
Mambo yanayochengua wudhuu´ ni yale mambo yanayoubatilisha ambapo akifanya moja wapo basi wudhuu´ wake unavunjika. Ni kama mfano wa mambo yanayochengua Uislamu kukikusudiwa yanayoubatilisha.
Manane – Mambo yanayochengua na kuvunja wudhuu´ ni manane. Mambo haya ni kwa mujibu wa madhehebu ya Hanaabilah. Mambo haya manane hakuna maafikiano juu yake.
1 – Kila kinachotoka kupitia tupu ya mbele au ya nyuma
Hichi ni kichenguzi cha kwanza miongoni mwa vichenguzi vya wudhuu´. Kinachotoka kupitia tupu ya mbele au ya nyuma ni kama mfano wa mkojo, kinyesi, manii, madhiy, wadiy na upepo. Mambo haya yanachengua wudhuu´ kwa maafikiano[1]. Kuna jopo kubwa la wanachuoni ambao hawaoni kuchenguka kwa wudhuu´ isipokuwa tu kwa kile chenye kutoka kupitia njia mbili hizi. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy (Rahimahu Allaah) katika “as-Swahiyh” yake[2] ameweka mlango ambapo akasema:
“Mlango wale wasioonelea kuchenguka kwa wudhuu´ isipokuwa kwa kile chenye kutoka kupitia tupu ya mbele na ya nyuma.”
[1] Tazama ”al-Ijmaa”, uk. 31 ya Ibn-ul-Mundhir.
[2] Kitaab-ul-Wudhuu´.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 33-35
Imechapishwa: 16/12/2021
https://firqatunnajia.com/23-kichenguzi-cha-kwanza-cha-wudhuu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)