Hadiyth ya nane
وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ
“Na utabakia uso wa Mola Wako wenye utukufu na wenye ukarimu.”[1]
100 – Abu ´Abdillaah Muhammad bin ´Aliy bin Wahb amenihadithia kwa kunisomea Kairo: Nilimsomea Abul-Hasan ash-Shaafi´iy: Abut-Twaahir as-Silafiy ametuhadithia: Abu ´Abdillaah ath-Thaqafiy ametuhadithia: ´Aliy bin Muhammad ametuhadithia: Ismaa´iyl as-Swaffaar ametuhadithia: Sa´daan ametuhadithia: Ibn ´Uyaynah ametuhadithia, kutoka kwa ´Amr ambaye ameeleza kuwa amemsikia Jaabir akisema:
”Wakati Aayah:
قُلْ هُوَ الْقَادِرُ عَلَىٰ أَن يَبْعَثَ عَلَيْكُمْ عَذَابًا مِّن فَوْقِكُمْ
“Sema: “Yeye ni muweza wa kukutumieni adhabu kutoka juu yenu… ”
ilipoteremshwa kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), alisema:
”Najilinda na uso Wako.”
na:
أَوْ مِن تَحْتِ أَرْجُلِكُمْ
”… au kutoka chini ya miguu yenu… ”
akasema:
”Najilinda na uso Wako.”
na:
أَوْ يَلْبِسَكُمْ شِيَعًا وَيُذِيقَ بَعْضَكُم بَأْسَ بَعْضٍ
”… au akutatanisheni mfarikiane kuwa makundimakundi na akuonjesheni baadhi yenu nguvu za wengineo.”[2]
Akasema: ”Afadhali haya mawili au ni mepesi.”[3]
Hadiyth ni Swahiyh.
101 – Miongoni mwa maudhui hayo ni kwamba Abu Muusa al-Ash´ariy (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alituhutubia mambo matano na kusema: “Allaah halali na wala haimstahikii Yeye kulala. Anaishusha mizani na kuinyanyua. Kwake kunapandishwa matendo ya usiku kabla ya mchana na matendo ya mchana kabla ya usiku. Pazia Yake ni Nuru; lau ataifunua, basi mwanga wa uso Wake ungeliunguza kila anachoona katika uumbaji Wake.”[4]
102 – Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema tena:
”Hakika Mola wenu hana usiku wala mchana. Nuru ya mbingu na ardhi inatokana na nuru ya uso Wake.”
103 – Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
اللهم إني أَسْأَلكَ لَذَّةَ النَّظرِ إِلى وَجْهِكَ وَالشَّوْقَ إِلَى لِقَائِكَ
”Ee Allaah! Hakika mimi nakuomba ladha ya kutazama uso Wako na kutamani kukutana Nawe.”[5]
104 – Ibn Mas´uud amesema:
”Mwenye kusema:
سبحان الله و الحمد لله و الله اكبر
”Allaah ametakasika kutokana na mapungufu, himdi zote njema anastahiki Allaah na Allaah ni mkubwa.”,
anayapokea Malaika na kumpelekea nayo Allaah (Ta´ala). Hapiti kundi lolote la Malaika isipokuwa wanamuombea msamaha aliyeyatamka mpaka wafike nayo kwenye uso wa Allaah.”
105 – Abu Bakr as-Swiddiyq, Hudhayfah, Abu Muusa na Maswahabah wengine (Radhiya Allaahu ´anhum) wamesema kuhusu maneno Yake Allaah (Ta´ala):
لِّلَّذِينَ أَحْسَنُوا الْحُسْنَىٰ وَزِيَادَةٌ
“Kwa wale waliofanya mazuri watapata Pepo na zaidi.”[6]
”Watatazama uso wa Allaah (Ta´ala).”[7]
Allaah (Ta´ala) amesema:
وكُلُّ شَيْءٍ هَالِكٌ إِلَّا وَجْهَهُ
“Kila kitu ni chenye kuangamia isipokuwa uso Wake.”[8]
[1]55:27
[2] 6:65
[3] Muslim (179).
[4] Muslim (179).
[5] an-Nasaa’iy (1305) na ni Swahiyh kwa mujibu wa Ibn Hibbaan (509 – al-Mawaarid) na al-Albaaniy katika ”as-Sunnah” (424).
[6] 10:26
[7] Jaamiy´-ul-Bayaan (12/155-165).
[8] 28:88
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy (afk. 748)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 105-109
- Imechapishwa: 09/06/2024
Hadiyth ya nane
وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ
“Na utabakia uso wa Mola Wako wenye utukufu na wenye ukarimu.”[1]
100 – Abu ´Abdillaah Muhammad bin ´Aliy bin Wahb amenihadithia kwa kunisomea Kairo: Nilimsomea Abul-Hasan ash-Shaafi´iy: Abut-Twaahir as-Silafiy ametuhadithia: Abu ´Abdillaah ath-Thaqafiy ametuhadithia: ´Aliy bin Muhammad ametuhadithia: Ismaa´iyl as-Swaffaar ametuhadithia: Sa´daan ametuhadithia: Ibn ´Uyaynah ametuhadithia, kutoka kwa ´Amr ambaye ameeleza kuwa amemsikia Jaabir akisema:
”Wakati Aayah:
قُلْ هُوَ الْقَادِرُ عَلَىٰ أَن يَبْعَثَ عَلَيْكُمْ عَذَابًا مِّن فَوْقِكُمْ
“Sema: “Yeye ni muweza wa kukutumieni adhabu kutoka juu yenu… ”
ilipoteremshwa kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), alisema:
”Najilinda na uso Wako.”
na:
أَوْ مِن تَحْتِ أَرْجُلِكُمْ
”… au kutoka chini ya miguu yenu… ”
akasema:
”Najilinda na uso Wako.”
na:
أَوْ يَلْبِسَكُمْ شِيَعًا وَيُذِيقَ بَعْضَكُم بَأْسَ بَعْضٍ
”… au akutatanisheni mfarikiane kuwa makundimakundi na akuonjesheni baadhi yenu nguvu za wengineo.”[2]
Akasema: ”Afadhali haya mawili au ni mepesi.”[3]
Hadiyth ni Swahiyh.
101 – Miongoni mwa maudhui hayo ni kwamba Abu Muusa al-Ash´ariy (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alituhutubia mambo matano na kusema: “Allaah halali na wala haimstahikii Yeye kulala. Anaishusha mizani na kuinyanyua. Kwake kunapandishwa matendo ya usiku kabla ya mchana na matendo ya mchana kabla ya usiku. Pazia Yake ni Nuru; lau ataifunua, basi mwanga wa uso Wake ungeliunguza kila anachoona katika uumbaji Wake.”[4]
102 – Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema tena:
”Hakika Mola wenu hana usiku wala mchana. Nuru ya mbingu na ardhi inatokana na nuru ya uso Wake.”
103 – Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
اللهم إني أَسْأَلكَ لَذَّةَ النَّظرِ إِلى وَجْهِكَ وَالشَّوْقَ إِلَى لِقَائِكَ
”Ee Allaah! Hakika mimi nakuomba ladha ya kutazama uso Wako na kutamani kukutana Nawe.”[5]
104 – Ibn Mas´uud amesema:
”Mwenye kusema:
سبحان الله و الحمد لله و الله اكبر
”Allaah ametakasika kutokana na mapungufu, himdi zote njema anastahiki Allaah na Allaah ni mkubwa.”,
anayapokea Malaika na kumpelekea nayo Allaah (Ta´ala). Hapiti kundi lolote la Malaika isipokuwa wanamuombea msamaha aliyeyatamka mpaka wafike nayo kwenye uso wa Allaah.”
105 – Abu Bakr as-Swiddiyq, Hudhayfah, Abu Muusa na Maswahabah wengine (Radhiya Allaahu ´anhum) wamesema kuhusu maneno Yake Allaah (Ta´ala):
لِّلَّذِينَ أَحْسَنُوا الْحُسْنَىٰ وَزِيَادَةٌ
“Kwa wale waliofanya mazuri watapata Pepo na zaidi.”[6]
”Watatazama uso wa Allaah (Ta´ala).”[7]
Allaah (Ta´ala) amesema:
وكُلُّ شَيْءٍ هَالِكٌ إِلَّا وَجْهَهُ
“Kila kitu ni chenye kuangamia isipokuwa uso Wake.”[8]
[1]55:27
[2] 6:65
[3] Muslim (179).
[4] Muslim (179).
[5] an-Nasaa’iy (1305) na ni Swahiyh kwa mujibu wa Ibn Hibbaan (509 – al-Mawaarid) na al-Albaaniy katika ”as-Sunnah” (424).
[6] 10:26
[7] Jaamiy´-ul-Bayaan (12/155-165).
[8] 28:88
Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy (afk. 748)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 105-109
Imechapishwa: 09/06/2024
https://firqatunnajia.com/23-hadiyth-najilinda-na-uso-wako/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)