Miongoni mwa waliosema kwamba Allaah yuko juu ya ´Arshi kwa dhati Yake ni Imaam Yahyaa bin ´Ammaar na Imaam Abu Naswr as-Sijziy, ambaye amesema katika kitabu “al-Ibaanah”:
“Maimamu wetu kama ath-Thawriy, Maalik, Ibn ´Uyaynah, Hammaad bin Salamah, Hammaad bin Zayd, Ibn-ul-Mubaarak, al-Fudhwayl bin ´Iyaadhw, Ahmad na Ishaaq, wameafikiana ya kwamba Allaah yuko juu ya ´Arshi kwa dhati Yake na kwamba ujuzi Wake uko kila sehemu.”
Hivyo hivyo kasema Shaykh-ul-Islaam al-Answariy:
“Kuna mapokezi mengi yanayosema kuwa Allaah yuko juu ya mbingu ya saba juu ya ´Arshi.”
Hivyo pia ndivo kasema rafiki yake Abul-Hasan al-Karajiy katika utenzi wake kuhusu ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah:
´Aqiydah yao ni kwamba Mola kwa dhati Yake
yuko juu ya ´Arshi, pamoja na utambuzi Wake wa mambo ya ghaibu
Imaam Abul-Qaasim al-Laalakaa’iy ash-Shaafi´iy amesema:
“Mapokezi cha yale yaliyopokelewa kuhusiana na maneno Yake (Ta´ala):
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
”Mwingi wa rehema amelingana juu ya ´Arshi.”[1]
na kwamba Allaah yuko juu ya ´Arshi Yake juu ya mbingu.
Amesema (´Azza wa Jall):
إِلَيْهِ يَصْعَدُ الْكَلِمُ الطَّيِّبُ وَالْعَمَلُ الصَّالِحُ يَرْفَعُهُ
“Kwake linapanda neno zuri na tendo zuri hulitukuza.”[2]
أَأَمِنتُم مَّن فِي السَّمَاءِ أَن يَخْسِفَ بِكُمُ الْأَرْضَ
“Je, mnadhani mko katika amani na aliyeko juu mbinguni kwamba hatokudidimizeni ardhini?”[3]
وَهُوَ الْقَاهِرُ فَوْقَ عِبَادِهِ
“Naye ni Mwenye kutenza nguvu juu ya waja Wake.”[4]
Aayah hizi zinathibitisha ya kwamba Yeye (´Azza wa Jall) yuko juu mbinguni na kwamba utambuzi Wake umezunguka kila maeneo.
Haya yamesimuliwa kutoka kwa Maswahabah wafuatao:
”´Umar, Ibn Mas´uud, Ibn ´Abbaas na Umm Salamah.”
Haya yamesimuliwa kutoka kwa wanafunzi wa Maswahabah wafuatao:
Rabiy´ah bin Abiy ´Abdir-Rahmaan, Sulaymaan at-Taymiy na Muqaatil bin Hayyaan.
Yamesemwa na wanazuoni kama:
Maalik bin Anas, Sufyaan ath-Thawriy na Ahmad bin Hanbal.”[5]
[1] 20:5
[2] 35:10
[3] 67:16
[4] 6:61
[5] Sharh Usuwl I´tiqaad Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah (3/387-402).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad bin ´Abdil-Haadiy al-Maqdisiy (afk. 744)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Kalaam ´alaa Mas-alat-il-Istiwaa’ ´alaal-´Arsh, uk. 78-80
- Imechapishwa: 29/12/2025
Miongoni mwa waliosema kwamba Allaah yuko juu ya ´Arshi kwa dhati Yake ni Imaam Yahyaa bin ´Ammaar na Imaam Abu Naswr as-Sijziy, ambaye amesema katika kitabu “al-Ibaanah”:
“Maimamu wetu kama ath-Thawriy, Maalik, Ibn ´Uyaynah, Hammaad bin Salamah, Hammaad bin Zayd, Ibn-ul-Mubaarak, al-Fudhwayl bin ´Iyaadhw, Ahmad na Ishaaq, wameafikiana ya kwamba Allaah yuko juu ya ´Arshi kwa dhati Yake na kwamba ujuzi Wake uko kila sehemu.”
Hivyo hivyo kasema Shaykh-ul-Islaam al-Answariy:
“Kuna mapokezi mengi yanayosema kuwa Allaah yuko juu ya mbingu ya saba juu ya ´Arshi.”
Hivyo pia ndivo kasema rafiki yake Abul-Hasan al-Karajiy katika utenzi wake kuhusu ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah:
´Aqiydah yao ni kwamba Mola kwa dhati Yake
yuko juu ya ´Arshi, pamoja na utambuzi Wake wa mambo ya ghaibu
Imaam Abul-Qaasim al-Laalakaa’iy ash-Shaafi´iy amesema:
“Mapokezi cha yale yaliyopokelewa kuhusiana na maneno Yake (Ta´ala):
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
”Mwingi wa rehema amelingana juu ya ´Arshi.”[1]
na kwamba Allaah yuko juu ya ´Arshi Yake juu ya mbingu.
Amesema (´Azza wa Jall):
إِلَيْهِ يَصْعَدُ الْكَلِمُ الطَّيِّبُ وَالْعَمَلُ الصَّالِحُ يَرْفَعُهُ
“Kwake linapanda neno zuri na tendo zuri hulitukuza.”[2]
أَأَمِنتُم مَّن فِي السَّمَاءِ أَن يَخْسِفَ بِكُمُ الْأَرْضَ
“Je, mnadhani mko katika amani na aliyeko juu mbinguni kwamba hatokudidimizeni ardhini?”[3]
وَهُوَ الْقَاهِرُ فَوْقَ عِبَادِهِ
“Naye ni Mwenye kutenza nguvu juu ya waja Wake.”[4]
Aayah hizi zinathibitisha ya kwamba Yeye (´Azza wa Jall) yuko juu mbinguni na kwamba utambuzi Wake umezunguka kila maeneo.
Haya yamesimuliwa kutoka kwa Maswahabah wafuatao:
”´Umar, Ibn Mas´uud, Ibn ´Abbaas na Umm Salamah.”
Haya yamesimuliwa kutoka kwa wanafunzi wa Maswahabah wafuatao:
Rabiy´ah bin Abiy ´Abdir-Rahmaan, Sulaymaan at-Taymiy na Muqaatil bin Hayyaan.
Yamesemwa na wanazuoni kama:
Maalik bin Anas, Sufyaan ath-Thawriy na Ahmad bin Hanbal.”[5]
[1] 20:5
[2] 35:10
[3] 67:16
[4] 6:61
[5] Sharh Usuwl I´tiqaad Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah (3/387-402).
Muhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad bin ´Abdil-Haadiy al-Maqdisiy (afk. 744)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Kalaam ´alaa Mas-alat-il-Istiwaa’ ´alaal-´Arsh, uk. 78-80
Imechapishwa: 29/12/2025
https://firqatunnajia.com/22-yuko-juu-ya-mbingu-kwa-dhati-yake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket