Swali 22: Alifikwa na yepi yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na watu wa nyumbani kwake kutoka kwa washirikina wa ki-Quraysh?
Jibu: Washirikina hawakuacha kumuudhi mpaka mwishowe wakaafikiana kumuua. Allaah akamlinda kwa ami yake Abu Twaalib ambaye akaikusanya familia yake na ukoo wake Banuu Haashim na Banuu ´Abdil-Muttwalib. Makafiri na waumini wao wote wakaafikiana kumtetea Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kumtanguliza yeye mbele ya nafsi zao. Mtu pekee aliyepinga alikuwa Abu Lahab – iangamie mikono yake miwili!
- Mhusika: ´Allaamah Haafidhw bin Ahmad al-Hakamiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Amaaliy fiys-Siyrah an-Nabawiyyah, uk. 97-98
- Imechapishwa: 18/09/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)