10 – Upokezi wa Sahnuun[1] kutoka kwa maswahiba zake Maalik
Ibn Rushd amesema:
“Sahnuun akasema: “Mmoja wa marafiki zake Maalik amenikhabarisha kwamba alikuwa kwa Maalik wakati mtu mmoja alipomjia na kusema: “Ee Abu ´Abdillaah, nina swali.” Akakaa kimya. Akasema kwa mara nyingine: “Ee Abu ´Abdillaah, nina swali.” Akaendelea kukaa kimya. Akauliza kwa mara ya tatu, ambapo Maalik akainua kichwa kwa lengo la kumjibu. Akasema: “Ee Abu ´Abdillaah!
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
”Mwingi wa rehema amelingana juu ya ´Arshi.”[2]
Ilikuweje kulingana Kwake juu?” Maalik akainamisha kichwa chake kwa muda kisha akakiinua na kusema: ”Umeuliza juu ya kitu ambacho si kwamba hakitambuliki na umezungumzia kisichofahamika. Sikuoni vyengine isipokuwa mtu muovu. Mtoeni nje!”[3]
[1] Imaam, ´Allaamah na mwanachuoni wa Afrika Kaskazini, Abu Sa’iyd ´Abdus-Salaam bin Habiyb bin Hassaan at-Tannuukhiy. Jaji wa Qayrawaan na mtunzi wa “al-Mudawwanah”.
Amesikia kutoka kwa Sufyaan bin ´Uyaynah na akalazimiana na wanafunzi wa Maalik Ibn Wahb, Ibn-ul-Qaasim na Ash-hab mpaka akawa analingana nao. Alikufa mwaka 240. Tazama “Siyar A´laam-in-Nubalaa’” (12/63-69).
[2] 20:05
[3] al-Bayaan wat-Tahswiyl (16/367-369).
- Muhusika: Shaykh ´Abdur-Razzaaq bin ´Allaamah ´Abdil-Muhsin al-´Abbaad al-Badr
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Athar al-Mash-huur ´an-il-Imaam Maalik fiy Swifat-il-Istiwaa’, uk. 41
- Imechapishwa: 30/11/2025
10 – Upokezi wa Sahnuun[1] kutoka kwa maswahiba zake Maalik
Ibn Rushd amesema:
“Sahnuun akasema: “Mmoja wa marafiki zake Maalik amenikhabarisha kwamba alikuwa kwa Maalik wakati mtu mmoja alipomjia na kusema: “Ee Abu ´Abdillaah, nina swali.” Akakaa kimya. Akasema kwa mara nyingine: “Ee Abu ´Abdillaah, nina swali.” Akaendelea kukaa kimya. Akauliza kwa mara ya tatu, ambapo Maalik akainua kichwa kwa lengo la kumjibu. Akasema: “Ee Abu ´Abdillaah!
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
”Mwingi wa rehema amelingana juu ya ´Arshi.”[2]
Ilikuweje kulingana Kwake juu?” Maalik akainamisha kichwa chake kwa muda kisha akakiinua na kusema: ”Umeuliza juu ya kitu ambacho si kwamba hakitambuliki na umezungumzia kisichofahamika. Sikuoni vyengine isipokuwa mtu muovu. Mtoeni nje!”[3]
[1] Imaam, ´Allaamah na mwanachuoni wa Afrika Kaskazini, Abu Sa’iyd ´Abdus-Salaam bin Habiyb bin Hassaan at-Tannuukhiy. Jaji wa Qayrawaan na mtunzi wa “al-Mudawwanah”.
Amesikia kutoka kwa Sufyaan bin ´Uyaynah na akalazimiana na wanafunzi wa Maalik Ibn Wahb, Ibn-ul-Qaasim na Ash-hab mpaka akawa analingana nao. Alikufa mwaka 240. Tazama “Siyar A´laam-in-Nubalaa’” (12/63-69).
[2] 20:05
[3] al-Bayaan wat-Tahswiyl (16/367-369).
Muhusika: Shaykh ´Abdur-Razzaaq bin ´Allaamah ´Abdil-Muhsin al-´Abbaad al-Badr
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Athar al-Mash-huur ´an-il-Imaam Maalik fiy Swifat-il-Istiwaa’, uk. 41
Imechapishwa: 30/11/2025
https://firqatunnajia.com/22-masimulizi-ya-maalik-kwa-mujibu-wa-wasimulizi-kutoka-kwa-maswahiba-wa-maalik/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
