Swali 21: Salaf wanapowakufurisha watu maalum wa madhehebu ya Jahmiyyah, kama ambavo ash-Shaafi´iy alivyomkufurisha Hafsw al-Fard wakati aliposema kuwa Qur-aan ni kiumbe, ambapo ash-Shaafi´iy akamwambia kuwa amemkufuru Allaah Mtukufu, kama alivyonukuu al-Laalakaa’iy katika ”Sharh Usuul I’tiqaad Ahl-is-Sunnah”, na kama walivyokafirishwa Jahm bin Swafwaan, Bishr al-Maariysiy, an-Nadhwaam na Abul-Hudhayl al-‘Allaaf, kama alivyonukuu Ibn Battwah katika ”al-Ibaanah as-Sughraa” – Je, wanakusudia kuwakufurisha watu hawa wenyewe kama wenyewe au maneno yao ndio ya kikafiri na si wao kama wao?
Jibu: Dhahiri ni kwamba kinachokusudiwa ni kuwakufurisha wao kama wao kutokana na kutajwa majina yao kwa upekee. Vivyo hivyo kinachohihiri ni kwamba ash-Shaafi´iy alimjadili na akasimamisha hoja dhidi yake. Kunapokusudiwa kukufurisha kwa ujumla ni kama pale baadhi yao wanaposema:
”Jahmiyyah ni makafiri.”
Lakini pale wanapobainishwa watu maalum waliokabiliana na maimamu na kujadiliana nao, makusudio inakuwa kuwakufurisha wao kama wao. Wanazuoni wana mitazamo tofauti kuhusu kuwakufurisha Jahmiyyah:
1 – Wako wenye kuona kuwa wale waliochupa mipaka ni makafiri.
2 – Wengine wakaona kuwa wote ni makafiri.
3 – Wengine wakaona kuwa wote ni wazushi.
Inapokuja kwa wale mmojammoja ambao waliwakabili maimamu na wakajadiliana nao, udhahiri ni kwamba waliwakufurisha wao kama wao kwa sababu hoja inakuwa imesimama dhidi yao.
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: As-ilah wa Ajwibah fiy-Iymaan wal-Kufr, uk. 51
- Imechapishwa: 08/01/2026
Swali 21: Salaf wanapowakufurisha watu maalum wa madhehebu ya Jahmiyyah, kama ambavo ash-Shaafi´iy alivyomkufurisha Hafsw al-Fard wakati aliposema kuwa Qur-aan ni kiumbe, ambapo ash-Shaafi´iy akamwambia kuwa amemkufuru Allaah Mtukufu, kama alivyonukuu al-Laalakaa’iy katika ”Sharh Usuul I’tiqaad Ahl-is-Sunnah”, na kama walivyokafirishwa Jahm bin Swafwaan, Bishr al-Maariysiy, an-Nadhwaam na Abul-Hudhayl al-‘Allaaf, kama alivyonukuu Ibn Battwah katika ”al-Ibaanah as-Sughraa” – Je, wanakusudia kuwakufurisha watu hawa wenyewe kama wenyewe au maneno yao ndio ya kikafiri na si wao kama wao?
Jibu: Dhahiri ni kwamba kinachokusudiwa ni kuwakufurisha wao kama wao kutokana na kutajwa majina yao kwa upekee. Vivyo hivyo kinachohihiri ni kwamba ash-Shaafi´iy alimjadili na akasimamisha hoja dhidi yake. Kunapokusudiwa kukufurisha kwa ujumla ni kama pale baadhi yao wanaposema:
”Jahmiyyah ni makafiri.”
Lakini pale wanapobainishwa watu maalum waliokabiliana na maimamu na kujadiliana nao, makusudio inakuwa kuwakufurisha wao kama wao. Wanazuoni wana mitazamo tofauti kuhusu kuwakufurisha Jahmiyyah:
1 – Wako wenye kuona kuwa wale waliochupa mipaka ni makafiri.
2 – Wengine wakaona kuwa wote ni makafiri.
3 – Wengine wakaona kuwa wote ni wazushi.
Inapokuja kwa wale mmojammoja ambao waliwakabili maimamu na wakajadiliana nao, udhahiri ni kwamba waliwakufurisha wao kama wao kwa sababu hoja inakuwa imesimama dhidi yao.
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: As-ilah wa Ajwibah fiy-Iymaan wal-Kufr, uk. 51
Imechapishwa: 08/01/2026
https://firqatunnajia.com/21-makusudio-ya-takfiyr-ya-salaf-kwa-baadhi-ya-mapote-na-baadhi-ya-ahl-ul-bidah/