Kuna kitu nataka kukizindua. Mwanafunzi anatakiwa kutenga wakati wa kufanya marejeleo kwa yale aliyoyasoma. Ama mwanafunzi kujifunza kitu kisha akakisahau baada ya hapo na wala asikirudilii, hakika hili halimnufaishi kitu mwanafunzi.
Mwanafunzi anatakiwa kujipangia wakati wa kufanya marejeleo. Bora zaidi akifanya marejeleo na rafiki mwingine. Kwa mfano anaweza kutenga wakati wa kufanya marejeleo ya kila siku kwa njia ya kwamba kila siku baada ya kumaliza kusoma darsa fulani, anafanya marejeleo na rafiki yake kile alichokisoma na kila mmoja akaorodhesha vipengele vya faida alivyojifunza. Kisha afanye marejeleo ya wiki. Kwa mfano atenge wakati siku ya ijumaa ambapo anarudilia yale aliyofaidika katika wiki hii. Kisha afanye marejeleo ya mwezi. Kwa mfano atenge siku moja katika mwezi ambapo anarudilia yale aliyojifunza. Aendelee namna hii. Hivi ndivyo walivyokuwa wakifanya Salaf.
- Muhusika: Shaykh Sulaymaan bin Saliymillaah ar-Ruhayliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-´Ilm wa Wasaaailuh wa Thimaaruh
- Imechapishwa: 22/10/2016
Kuna kitu nataka kukizindua. Mwanafunzi anatakiwa kutenga wakati wa kufanya marejeleo kwa yale aliyoyasoma. Ama mwanafunzi kujifunza kitu kisha akakisahau baada ya hapo na wala asikirudilii, hakika hili halimnufaishi kitu mwanafunzi.
Mwanafunzi anatakiwa kujipangia wakati wa kufanya marejeleo. Bora zaidi akifanya marejeleo na rafiki mwingine. Kwa mfano anaweza kutenga wakati wa kufanya marejeleo ya kila siku kwa njia ya kwamba kila siku baada ya kumaliza kusoma darsa fulani, anafanya marejeleo na rafiki yake kile alichokisoma na kila mmoja akaorodhesha vipengele vya faida alivyojifunza. Kisha afanye marejeleo ya wiki. Kwa mfano atenge wakati siku ya ijumaa ambapo anarudilia yale aliyofaidika katika wiki hii. Kisha afanye marejeleo ya mwezi. Kwa mfano atenge siku moja katika mwezi ambapo anarudilia yale aliyojifunza. Aendelee namna hii. Hivi ndivyo walivyokuwa wakifanya Salaf.
Muhusika: Shaykh Sulaymaan bin Saliymillaah ar-Ruhayliy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-´Ilm wa Wasaaailuh wa Thimaaruh
Imechapishwa: 22/10/2016
https://firqatunnajia.com/20-kutenga-wakati-wa-kufanya-marejeleo/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)